Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Esther Edwin Maleko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER E. MALLEKO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza mkakati wa ujenzi wa hosteli kwenye shule za kata?

Supplementary Question 1

MHE. ESTHER E. MALLEKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana, pamoja na majibu mazuri ya Serikali naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Katika kuboresha ufaulu katika shule zetu za kata; je, Serikali ina mpango gani sasa kuweza kukamilisha maabara?

Lakini swali la pili, ni lini Serikali itamaliza upungufu wa walimu hasa wa sayansi katika shule zetu za Mkoa wa Kilimanjaro?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili madogo ya nyongeza ya Mheshimiwa Esther Edwin Malleko, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la kwanza ni kwamba lengo la Serikali kwa sasa ni kuhakikisha shule zote zinakuwa na maabara na ndiyo maana katika kila mwaka wa fedha tumetenga fedha kujenga maabara katika shule zetu za sekondari za kata nchini. Kwa hiyo, hilo ni kipaumbele chetu ambacho Mheshimiwa Rais Mama Samia Suluhu Hassan ametuagiza.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili, upungufu wa walimu wa sayansi tunautambua na ndiyo maana katika ajira zote ambazo tumekuwa tukizitoa sasa hivi tunawapa vipaumbele pia zaidi walimu ambao wamesoma masomo ya sayansi na tutaendelea kufanya hivyo ili kuondoa hili tatizo la uhaba wa walimu wa sayansi katika shule zetu. Ahsante sana.

Name

Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. ESTHER E. MALLEKO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza mkakati wa ujenzi wa hosteli kwenye shule za kata?

Supplementary Question 2

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana; je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha kwamba shule zote za kata na za Serikali kwa ujumla zinapata hatimiliki?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Profesa Ndakidemi, Mbunge wa Jimbo la Moshi Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, lengo la Serikali ni kuhakikisha shule zote zinakuwa na hati iliki na ndiyo mpango uliopo sasa na tumehamasisha halmashauri zote kutekeleza jambo hilo. Kwa hiyo lipo katika mpango wa Serikali. Ahsante.