Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 7 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 96 2022-09-21

Name

Esther Edwin Maleko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER E. MALLEKO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza mkakati wa ujenzi wa hosteli kwenye shule za kata?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Esther Edwin Malleko, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua umuhimu wa shule kuwa karibu na jamii na kwa muktadha huo Serikali ilielekeza kujengwa kwa shule za kata nchi nzima ili kuwawezesha wanafunzi kusoma karibu na maeneo wanayoishi.

Mheshimiwa Naibu Spika, utaratibu uliopo kwa sasa wa ujenzi wa hosteli kwenye shule za kata ambazo kulingana na jiografia ya eneo hususani umbali kutoka shule na makazi ya watu wananchi wenyewe wamekuwa wakijenga hosteli hizo na kuweka utaratibu wa kuziendesha na kuzisimamia kulingana na mahitaji waliyonayo.