Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza: - Je, kwa takwimu ni wahitimu wangapi wa kada ya Ualimu wa masomo ya sayansi na hesabu hawajaajiriwa tangu mwaka 2015?

Supplementary Question 1

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Dunia ya sasa ni ya sayansi na teknolojia, hivyo kama Taifa lazima tuwekeze kuhakikisha kwamba tunakuwa na Walimu wa kutosha kwenye masomo haya ya sayansi na hesabu; na kwa kuwa kuna uhaba mkubwa sana wa Walimu waliopo ni takribani asilimia 33 tu. Je, ni nini mkakati madhubuti na wa haraka wa Serikali wa kuhakikisha kwamba inaajiri Walimu wa kutosha ili kukabiliana na changamoto hii?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; kwa kuwa wahitimu hawa ambao hawajaajiriwa tangu mwaka 2015 ni takribani asilimia 60 na wengi wao wamekuwa wakijitolea kufundisha bila ajira rasmi. Ni kwa nini Serikali isiwape kipaumbele Walimu hawa wanaojitolea kwa kuwaajiri kwenye maeneo ambayo wanajitolea kwa sasa?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Esther Nicholaus Matiko, Mbunge wa Viti Maalum, kwa pamoja kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Matiko kwa ufatiliaji wa karibu wa Walimu wetu wa masomo ya sayansi pamoja na hisabati. Hata hivyo, kama nilivyokwishaeleza kwenye majibu yangu ya msingi kwamba Serikali imeendelea kutoa fursa za ajira kwa Walimu hawa, tunajua changamoto ipo na uhitaji upo ni mkubwa. Nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba Ofisi ya Rais, TAMISEMI yenye dhamana ya kuomba vibali tayari katika mwaka huu wa fedha imeshaomba kibali cha kuajiri Walimu zaidi ya 42,697 ambapo kipaumbele kikubwa sana tutawapa Walimu wa sayansi pamoja na hisabati na wale ambao wanajitolea katika maeneo mbalimbali nchini. Nakushukuru sana.