Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Deus Clement Sangu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. DEUS C. SANGU aliuliza: - Je, nini mpango wa kujenga Skimu ya umwagiliaji Kata za Kaoze, Kipeta na Kilangawana kwa kutumia Mto Momba Kwela?

Supplementary Question 1

MHE. DEUS C. SANGU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Pamoja na majibu yenye matumaini kutoka Serikalini, naomba niulize maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, utambuzi wa Bonde la Mititi na Ilembo ndani ya Jimbo la Kwela kwa ajili ya kuanzisha skimu umefanyika muda mrefu. Sasa nataka kujua, ni lini Serikali mtaleta fedha kwa ajili ya usanifu kuanzisha skimu hizo?

Swali la pili; skimu ya umwagiliaji iliyopo Kata ya Ilemba kwa maana ya Kijiji cha Sakalilo, imetumia muda mrefu sasa, imetumia zaidi ya Bilioni Moja, na bado fedha karibia Milioni 800 kukamilisha skimu hiyo. Nataka kujua ni lini wataleta fedha hiyo ili iweze kukamilisha skimu hii ya Sakalilo?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Deus Clement Sangu, Mbunge wa Kwela, kwa pamoja kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Spika, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba mipango hiyo tumeiweka katika Mwaka wa Fedha 2023/2024 na imekuwa ni kilio cha Mheshimiwa Mbunge. Ahadi yetu ni kwamba tutafanya utekelezaji katika mwaka huu wa fedha na kuendelea.

Name

Ally Anyigulile Jumbe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Primary Question

MHE. DEUS C. SANGU aliuliza: - Je, nini mpango wa kujenga Skimu ya umwagiliaji Kata za Kaoze, Kipeta na Kilangawana kwa kutumia Mto Momba Kwela?

Supplementary Question 2

MHE. ALLY A. J. M. JUMBE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri, ni lini Mkandarasi wa kujenga Skimu ya Umwagiliaji ya Makwale Wilayani Kyela kutumia Mto Rufilio ataanza kazi?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ally Jumbe, Mbunge wa Kyela, kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Spika, maelekezo ambayo tuliyatoa kwa Wakandarasi wote wale ambao walisaini mikataba wakati wa sherehe ya Nanenane pale Mbeya ni kwamba wanapaswa kuwa site kuanzia tarehe 15. Lakini tu nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kwa hoja yake mahsusi, basi tutahakikisha kwamba tunamharakisha Mkandarasi huyo aende kuanza kazi mapema kama ambavyo maelekezo yalitoka Wizarani.

Name

Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. DEUS C. SANGU aliuliza: - Je, nini mpango wa kujenga Skimu ya umwagiliaji Kata za Kaoze, Kipeta na Kilangawana kwa kutumia Mto Momba Kwela?

Supplementary Question 3

MHE. DENNIS L. LONDO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa ardhi ambayo inafaa kwa umwagiliaji ambayo inatumika sasa hivi kwa miradi ya umwagiliaji ni pungufu ya asilimia Tano. Je, nini mkakati wa Serikali kushirikisha sekta binafsi katika kuhakikisha maeneo yote ambayo yanafaa kwa umwagiliaji yanajengewa skimu? Nashukuru.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dennis Londo, Mbunge wa Mikumi, kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Spika, katika Jedwali Na. 6 la Kitabu cha Bajeti cha Wizara ya Kilimo, imeelezwa mahsusi kabisa kwamba Serikali imejipanga kuyafanyia upembuzi yakinifu na usanifu mabonde yote makubwa 22 ndani ya Nchi yetu ya Tanzania kuhakikisha yote yanafanya kilimo cha umwagiliaji, yakiwemo mabonde ya Mto Songwe, Ifakara, Idete, Pangani, Rufiji, Chamanzi na Malagarasi pamoja na Ziwa Victoria.

Name

George Natany Malima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. DEUS C. SANGU aliuliza: - Je, nini mpango wa kujenga Skimu ya umwagiliaji Kata za Kaoze, Kipeta na Kilangawana kwa kutumia Mto Momba Kwela?

Supplementary Question 4

MHE. GEORGE N. MALIMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi. Naishukuru Serikali kwa kutoa fedha kuchimba bwawa la umwagiliaji katika Kata ya Chunyu, Namhambi: Je, ni lini kazi hii itaanza?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa George Malima, Mbunge wa Mpwapwa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mkandarasi anayejenga mradi wa skimu ya umwagiliaji ya Msagali, hivi sasa yuko site ameanza mobilization na ni kati ya wale Wakandarasi 21 ambao walisaini mikataba pale Nanenane Mbeya na tunategemea muda wowote aanze kazi hiyo. Vile vile bwawa ambalo linajengwa pale likikamilika litakuwa na uwezo wa kutoa lita za mita za ujazo milioni 92. Kwa hiyo, ni habari njema kwa wana-Mpwapwa na kwa bahati nzuri mkandarasi yuko site tayari. (Makofi)