Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 8 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 125 2022-09-22

Name

Deus Clement Sangu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. DEUS C. SANGU aliuliza: -

Je, nini mpango wa kujenga Skimu ya umwagiliaji Kata za Kaoze, Kipeta na Kilangawana kwa kutumia Mto Momba Kwela?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Deus Clement Sangu, Mbunge wa Kwela, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga Vijijini kwa kushirikiana na Tume ya Taifa ya Umwagiliaji imepanga kupima mabonde ya umwagiliaji yaliyopo katika Kata za Kaoze, Kipeta na Kilangawana ili kubaini eneo halisi linalofaa kwa kilimo cha umwagiliaji, pia ulalo wa ardhi, kiasi cha maji kwa ajili ya umwagiliaji na aina ya mioundombinu itakayohitajika.

Mheshimiwa Spika, upimaji huo utahusisha hekta 16,000 katika Kata ya Kaoze, hekta 5,000 katika Bonde la Kata ya Kipeta na hekta 7,000 katika Bonde la Maleza, Kata ya Kilangawana. Kukamilika kwa upimaji huo kutawezesha maeneo hayo kuingizwa kwenye mpango wa uendelezaji wa miundombinu ya umwagiliaji kwa kipindi cha mwaka 2023/2024 na kuendelea.