Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza: - Je, ni lini Mradi wa Maji wa Halmashauri 28 ambapo Njombe ni mojawapo utaanza kutekelezwa?

Supplementary Question 1

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuweza kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwanza tunaishukuru Serikali kwa hatua hizo za awali. Ili mradi uweze kwenda na wakati ni lazima yale maeneo ambayo mabomba yanapita yawe wazi. Na ili yale maeneo ambayo mabomba yanapita yawe wazi, lazima wananchi walipwe fidia.

Je, ni lini Serikali itawalipa fidia wananchi hao?

Swali langu la pili; je, ni lini mradi wa Igongwe wa Kata Nne za Jimbo la Njombe Mjini utapatiwa pesa ili Mkandarasi aendelee na kazi yake? Ahsante.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Neema Mgaya kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, awali ya yote ninampongeza Mheshimiwa Neema kwa ufuatiliaji. Suala la fidia tunaelekea kulipa kadri mradi unavyoendelea kujengwa na kila kitu kitakuwa kinakwenda kwa pamoja.

Mheshimiwa Spika, suala la mradi wa Igongwe kwenye Kata Nne, fedha zitaendelea kwenda kadiri tunavyozipata, na fedha ambazo zinafuata msimu ujao, huu mradi pia nao upo katika mpango.

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza: - Je, ni lini Mradi wa Maji wa Halmashauri 28 ambapo Njombe ni mojawapo utaanza kutekelezwa?

Supplementary Question 2

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Mradi wa Maji wa Izuga ni mradi wa muda mrefu, na kwa kuwa fedha iliyobaki ili mradi ukamilike ni milioni 76 tu. Kwa kuwa Mkandarasi yuko tayari walau apewe milioni 15 ili mradi ule ukamilike. Sasa, upo tayari baada ya Bunge hili mimi na wewe tuongozane mpaka Wizarani kuhakikisha kwamba Mkandarasi analipwa walau hiyo milioni 15 wananchi wapate maji? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, mkandarasi atalipwa, nami niko tayari kwenda naye site.

Name

Suma Ikenda Fyandomo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza: - Je, ni lini Mradi wa Maji wa Halmashauri 28 ambapo Njombe ni mojawapo utaanza kutekelezwa?

Supplementary Question 3

MHE. SUMA I. FYANDOMO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, ninaipongeza Serikali kwa kupata mkandarasi wa maji kwa ajili ya mradi wa Kiwira ambao utalisha wananchi wote wa Mkoa wa Mbeya. Sasa je, ni lini Serikali itatoa fedha ili mkandarasi aanze kufanya kazi mara moja?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali muhimu la nyongeza lililoulizwa na Mheshimiwa Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Mbeya, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, awali ya yote nimpongeze Mheshimiwa Suma kwa ufuatiliaji mzuri wa mradi huu muhimu ambao utakwenda kuleta manufaa kwa Mbeya Jiji na Wilaya jirani. Lini fedha inakwenda kupelekwa, tayari kazi zimeshaanza na Wizara tunafanya ununuzi na kupata Wakandarasi kwa sababu Mhandisi Mshauri ameshakamilisha kazi yake. Hadi kufikia Desemba mwaka huu mradi utaendelea na utekelezaji. Kwa hiyo, kwa kila hatua fedha inatolewa. Fedha ilishaanza kutolewa toka Februari na sasa hivi ipo katika maandalizi ya kumpata Mkandarasi.

Name

Shamsia Aziz Mtamba

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza: - Je, ni lini Mradi wa Maji wa Halmashauri 28 ambapo Njombe ni mojawapo utaanza kutekelezwa?

Supplementary Question 4

MHE. SHAMSIA A. MTAMBA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipatia nafasi ili nami niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itakamilisha mradi wa maji uliopo Kata ya Mango Pacha Nne ili kuwatua ndoo kichwani akina mama hawa ambao kwa muda mrefu, tokea tumepata uhuru, hawajawahi kabisa kufurahia huduma hii ya maji safi na salama? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Shamsia Mtamba, Mbunge wa Mtwara Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mradi utaendelea kuletewa fedha. Ninakupongeza Mheshimiwa Mbunge, ameshafuatilia sana huu mradi, fedha inakuja na mimi na wewe tutakwenda site kuhakikisha kazi inakamilika. Lengo ni kuona mwana mama anatua ndoo kichwani na ni dhamira safi ya Mheshimiwa Rais ambayo anayo kwa muda mrefu.

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza: - Je, ni lini Mradi wa Maji wa Halmashauri 28 ambapo Njombe ni mojawapo utaanza kutekelezwa?

Supplementary Question 5

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa kuwa Serikali ilitenga pesa kwa ajili ya ujenzi wa chujio la maji Wilayani Nyang’hwale kwenye bajeti ya 2022/2023 shilingi milioni 220.

Je, Serikali itatoa lini pesa hiyo na ujenzi uanze mara moja?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hussein Amar, Mbunge wa Nyang’hwale, kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Spika, nimpongeze Mheshimiwa Hussein kwa sababu tulishafuatilia awali, mradi sasa umefikia hatua nzuri. Suala la chujio, hizi milioni 200 zitaletwa kwa wakati, mgao ujao pia tutapunguza hii fedha, angalau milioni 100 ili kazi ziendelee kufanyika.

Name

Christopher Olonyokie Ole-Sendeka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Simanjiro

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza: - Je, ni lini Mradi wa Maji wa Halmashauri 28 ambapo Njombe ni mojawapo utaanza kutekelezwa?

Supplementary Question 6

MHE. CHRISTOPHER O. OLE-SENDEKA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa, utekelezaji wa agizo la Rais la kupeleka maji katika Kata Nne za Mererani, Endiamtu, Naisinyai, Shambarai na Oljoro Na. 5 umeanza katika Kata Mbili za Mererani na Indiamtu.

Je, ni lini sasa Wizara itatekeleza agizo hilo la Rais katika Kata zilizosalia kupitia Mradi ule Kabambe wa bilioni 400 wa Jiji la Arusha?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Christopher Ole-Sendeka, Mbunge wa Simanjiro, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, maagizo ya Mheshimiwa Rais kinachofuata ni utekelezaji, ndiyo maana katika Kata Nne tayari Mbili zimeshaanza kutekelezwa na Kata hizi Mbili pia lazima tuje tuzitekeleze ndani ya muda ambao Mheshimiwa Rais ametuagiza.

Name

Joseph Zacharius Kamonga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza: - Je, ni lini Mradi wa Maji wa Halmashauri 28 ambapo Njombe ni mojawapo utaanza kutekelezwa?

Supplementary Question 7

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, ninapenda kufahamu ni lini Serikali itapeleka maji Vijiji vya Kipingu na Kiogo ili kunusuru akina mama wanaoliwa sana na mamba? Ahsante.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kamonga kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Spika, Serikali tayari tunao utaratibu wa kwenda kuhakikisha maeneo ya Kiogo na maeneo yote kandokando ya Ziwa yanapata huduma ya maji safi na salama bombani ili kunusuru wananchi ambao wanaliwa na mamba. Tayari nimeshamuagiza Meneja wa Mkoa wa Njombe na ameshaniahidi ndani ya muda mfupi atahakikisha eneo ambalo mradi ulikuwa haujafika unakwenda kukamilika. (Makofi)

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza: - Je, ni lini Mradi wa Maji wa Halmashauri 28 ambapo Njombe ni mojawapo utaanza kutekelezwa?

Supplementary Question 8

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona, maana nimesimama muda mrefu sana.

Mheshimiwa Spika, katika Halmashauri ya Wilaya ya Chemba mwaka wa Fedha uliopita tulikuwa na miradi mitatu mikubwa. Mradi wa Machiga, Mradi wa Chandama na Mradi wa Visima 13, lakini mpaka leo wakandarasi wote hawako site; naomba kujua kauli ya Serikali juu ya Wakandarasi hawa. Ahsante.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Monni, Mbunge wa Chemba, kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Monni tumekuwa tukifanya kazi kwa pamoja na amefika Wizarani mara nyingi, nampongeza kwenye hilo. Miradi hii mikubwa ninaamini ameshaongea na Mheshimiwa Waziri, ameshaongea na Mheshimiwa Katibu Mkuu, tunakuja kutekeleza na Wakandarasi watafuata namna ambavyo wamesaini mikataba yao.(Makofi)