Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 8 Water and Irrigation Wizara ya Maji 124 2022-09-22

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza: -

Je, ni lini Mradi wa Maji wa Halmashauri 28 ambapo Njombe ni mojawapo utaanza kutekelezwa?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Neema William Mgaya, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifauatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali imeanza kutekeleza mradi wa maji wa Miji 28 ambapo Wakandarasi wote walisharipoti site mwezi Julai, 2022. Kwa sasa, Wakandarasi wanaendelea na usanifu wa kina na ujenzi wa miradi kwa Miji 28 ikiwemo Njombe utaanza mwezi Novemba, 2022.