Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nicodemas Henry Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA aliuliza: - Je, ni nini kauli ya Serikali juu ya askari wa misitu wanaopiga na kuwanyang’anya mkaa wananchi wa Mbogwe?

Supplementary Question 1

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA: Mheshimiwa Spika, ahsante, kwanza nashukuru kwa majibu ya Serikali, lakini naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza; Mawaziri wale nane walikuja Mkoani Geita, kule Mbongwe kuna changamoto ya migogoro ya watu wenye uhifadhi, kuna Kijiji kimoja cha Sango, majuzi kimewekewa vigingi katikati ambapo kilishapata GN toka mwaka 1976. Je, Waziri, msimamo huu ukoje, maana wananchi mpaka sasa hivi wana hofu kulingana na kigingi kilichowekwa?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, Mheshimiwa amesema kumekuwa na wimbo la ukataji wa mkaa, lakini kuna utaratibu wa kisheria hawa wananchi huwa wanazifuata. Ila kuna hawa Askari Mgambo ambao pengine hawana mafunzo vizuri ya kusimamia hizi sheria; kumekuwa na mgongano pale wanapofanya hizi operation wanawakamata wananchi ambapo wanavibali tayari lakini wanaonekana kuwaumiza na kutowatendea haki. Je, ni nini kauli ya Mheshimiwa Waziri ili kusudi wananchi hao pale wanapofuata sheria zote wafanye shughuli zao vizuri? (Makofi)

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Nicodemas Maganga, Mbunge wa Mbongwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli katika maeneo ya Mbongwe, baadhi ya vijiji vimeingizwa kwenye Kamati ya Mawaziri Nane na hivi ninayoongea tayari mikoa 13 imekwishatembelewa na maelekezo ya Serikali ni kwamba tunafanya tathmini na wataalam wako katika mikoa hiyo 13 wanafanya hizi tathmini, lakini pia kuona sasa namna ya maeneo ambayo yamehalalishwa kumegwa, yamegwe kwa ajili ya kuachia wananchi.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge, kwamba kwa kuwa maeneo hayo yako ndani ya tathmini ambayo inasimamiwa na Kamati ya Mawaziri Nane wa kisekta, tutaendelea kutoa maelekezo kwamba wananchi wasibughudhiwe wakati tunasubiri majibu ya tathmini hiyo. Kwa hiyo, vigingi visiwafanye wananchi wasifanye shughuli zao za kila siku, na hao wahifadhi tunawaelekeza wasilete vurugu yoyote mpaka pale ambapo tathmini ya Mawaziri nane itakapokamilisha kazi zake.

Mheshimiwa Spika, kauli ya Serikali kwa hawa wananchi ambao wanakutana na changamoto ya kukabiliana na askari pamoja na wananchi. Niendelee kutoa rai kwa wananchi, kwamba tuendelee kufuata sheria, taratibu na kanuni zinazosimamia uvunaji wa mazao ya misitu.

Mheshimiwa Spika, tumekuwa na changamoto, tunatoa vibali tukiamini kwamba vibali hivi vitatumika ipasavyo, lakini tumekuwa na changamoto ya uanzishwaji wa usafirishaji wa mazao ya misitu kwa kutumia pikipiki. Pikipiki inapita inaenda inavuna mti ambao haujaruhusiwa na wanapita njia zao za uchochoro, wakikamatwa wanasema wameonewa. Tuwaombe wafuate utaratibu na vibali vitolee kwa usahihi, ndivyo hawatakutana na changamoto ya kukamatwana na mazao haya ya misitu.

Name

Conchesta Leonce Rwamlaza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA aliuliza: - Je, ni nini kauli ya Serikali juu ya askari wa misitu wanaopiga na kuwanyang’anya mkaa wananchi wa Mbogwe?

Supplementary Question 2

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Licha ya kupewa vibali na sheria ilivyo lakini hawa askari, wakiwakamata watu hasa wenye baiskeli wanaobeba mkaa wanaharibu hata vyombo vyao vya usafiri. Je, Serikali inataka kutuambia kwamba sheria inaelekeza hivyo?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Askari wa Mazao ya Misitu wanapokuwa wanasimamia kwenye mageti, tuna changamoto kubwa sana ya usimamizi wa mazao haya. Ndani yake tuna askari wanaotoka kwenye halmashauri na kuna askari wanaotoka kwenye Wizara yetu ya Maliasili na Utalii. Kwa hiyo, kuna mkanganyiko hapa katikati ambao unajitokeza wakitaja maliasili, hata kama angekuwa ni Mgambo basi lawama inarudi Wizara ya Maliasili.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, niendelee kuwaomba wananchi, kwa kuwa tuna vyombo vya dola; pale ambapo unatendewa vivyo sivyo ripoti na taratibu za kisheria ziweze kuchukuliwa haraka.