Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 8 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 122 2022-09-22

Name

Nicodemas Henry Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA aliuliza: -

Je, ni nini kauli ya Serikali juu ya askari wa misitu wanaopiga na kuwanyang’anya mkaa wananchi wa Mbogwe?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Nicodemas Henry Maganga, Mbunge wa Mbogwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Askari wa Uhifadhi wanatekeleza majukumu yao kwa kuzingatia Sheria, Kanuni, miongozo na maelekezo ya viongozi mbalimbali ikiwemo ya Waheshimiwa Wabunge pamoja na kuzingatia haki za binadamu. Endapo kuna uvunjaji wa sheria, kanuni na miongozo iliyopo, Wizara haitosita kuwachukulia hatua watumishi wake wanaohusika na uvunjaji huo wa sheria.

Mheshimiwa Spika, kumekuwepo na wimbi la uvunaji wa mazao ya misitu, ukataji na uchomaji wa mkaa bila kufuata sheria, kanuni na taratibu zinazosimamia biashara hii. Hali hii imesababisha kutoweka kwa kasi kwa maeneo ya misitu na hatimaye kujitokeza kwa athari za mabadiliko ya tabia nchi. Hivyo, inapotokea mwananchi anasafirisha mazao ya misitu (mkaa) bila kufuata utaratibu, mazao hayo hutaifishwa na Serikali. Nitoe rai kwa wananchi wanaojishughulisha na biashara hiyo kufuata sheria, kanuni na taratibu husika.