Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENANI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka usafiri wa majini Ziwa Tanganyika?

Supplementary Question 1

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Nami niulize maswali mawili ya nyongeza. Nashukuru kwa majibu ya Serikali kwa hatua ya awali ya kutenga fedha, lakini sote tunajua; kutenga ni jambo moja na kutekeleza mpaka ujenzi ukamilike na meli ianze kutumika ni jambo lingine: Nataka kujua ni lini ujenzi wa meli hizo utakamilika na kuanza kutumika kwenye Ziwa Tanganyika? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili, Serikali imewekeza fedha kujenga Bandari ya Kasanga, Bandari ya Kabwe, Bandari ya Kipili, Bandari ya Kigoma pamoja na Karema, lakini hatuna usafiri wa uhakika wa Ziwa Tanganyika wa kubeba mizigo pamoja na mazao ambayo yanazalishwa kwenye hii mikoa mitatu. Nataka kujua kwa sababu huu muda ni mrefu wa kutengeneza hizo meli: Mna mpango wowote wa dharura wa kutuletea usafiri ili kuepusha tatizo la kila siku kupoteza maisha ya Watanzania kwa sababu ya kutumia maboti?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. FREDY A. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Aida Joseph Khenani, Mbunge wa Nkasi Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge kwa kufuatilia suala usafiri ndani ya Ziwa Tanganyika. Nami nimeshuhudia nilikwenda kule, kuna changamoto kubwa hiyo. Nataka nimhakikishie Mbunge na Wabunge wote wa mikoa yote mitatu; Mkoa wa Rukwa, Katavi pamoja na Kigoma, suala la kukamilika, kwanza kama ambavyo nimesema kwenye jibu langu la msingi, tumeshatangaza tenda tarehe 19 ya mwezi huu wa Tisa, tunategemea zitafunguliwa tarehe 2 Novemba na tayari Mheshimiwa Waziri wangu, Profesa Mbarawa alishakwenda kule kuonesha hata sehemu ya kujenga chelezo kwa kampuni ambazo zimeonesha kwamba zina nia ya kwenda kutengeneza ama kujenga hizi meli mpya mbili.

Mheshimiwa Spika, kwa swali la pili, kwamba ni namna gani tunaweza kama Serikali tukafanya jambo la dharura kwa ajili ya wananchi wa mikoa hii yote mitatu; kwanza, tumejipanga katika kukarabati meli zote mbili. Kuna meli ya Liemba pamoja na Mv Mwongozo. Tenda ya Mv Liemba, inatangazwa tarehe 26 ya mwezi huu na tunategemea kwamba itachukua muda wa mwaka mmoja. Kwa Mv Mwongozo ambayo inabeba abiria 500 na tani 150 yenyewe itachukua muda wa miezi sita. Kwa hiyo, ni mategemeo yetu kwamba ifikapo mwakani mwezi wa Kumi mwaka 2023 meli hizi za dharura zitakuwa zimeanza kufanya kazi ndani ya Ziwa Tanganyika. (Makofi)

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENANI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka usafiri wa majini Ziwa Tanganyika?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana. Nilitaka kujua, ni lini meli ya MV. Kaliasi itaanza tena safari zake kutoka Bandari ya Mwanza, Kwenda Bandari ya Nansio Visiwani Ukerewe? Nashukuru.

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. FREDY A. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mkundi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli tuna meli katika Ziwa Victoria ambayo ilipata shida katika mifumo yake ya kuongozea meli, na tulishaagiza kifaa hicho nje ya nchi; na ndani ya mwezi wa Kumi mwanzoni tunategemea kitakuja, kinaitwa mouse controller. Kwa hiyo, mwishoni mwa mwezi wa Kumi meli hii itaanza kufanya kazi zake ndani ya Ziwa Victoria. Ahsante sana.