Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 8 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 117 2022-09-22

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENANI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka usafiri wa majini Ziwa Tanganyika?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. FREDY A. MWAKIBETE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Aida Joseph Khenani, Mbunge wa Nkasi Kaskazini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali katika bajeti ya mwaka huu wa 2022/2023 imetenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa meli mbili mpya, chelezo na ukarabati wa meli za Mv Liemba na MT. Sangara ili kuboresha hali ya usafirishaji katika Ziwa Tanganyika. Kati ya meli zitakazojengwa, moja ni ya kubeba abiria 600 na tani 400 za mizigo na ya pili ni ya kubeba mabehewa na malori yenye uzito wa tani 3,000.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa Serikali kupitia Kampuni ya Huduma za Meli (MSCL) inaendelea na mchakato wa ununuzi wa Wakandarasi wa kutekeleza miradi hiyo.