Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA K.ny. MHE. FESTO R. SANGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Bwawa la Umeme la Mto Lumakali Wilayani Makete?

Supplementary Question 1

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Mimi na Mheshimiwa Festo Sanga tunaishukuru Serikali kwa hatua za awali kuhusiana na bwawa hili, lakini tulikuwa tunataka Serikali ituhakikishie ni lini wananchi wetu watalipwa fidia?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa wananchi wa Jimbo la Makete wamekuwa na changamoto kubwa sana ya kukatika katika kwa umeme kwa muda mrefu kwa sababu umeme huo unatoka Mbeya.

Je, Serikali inawahakikishia nini wananachi wa Makete kwamba bwawa hili litakuja kuwa tija ya kutatua changamoto hiyo? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza yaliyoulizwa na Mheshimiwa Neema Mgaya, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwenye swali la kwanza baada ya kukamilisha uthamini mwezi Oktoba ndiyo sasa taratibu za malipo zitaanza ikiwa ni kupelekea Mthamini Mkuu wa Serikali na fedha tayari imeshatengwa. Kwa hiyo, baada ya kukamilisha taratibu hizo fedha italipwa, tunaamini kabla ya kufikia mwanzoni mwa mwaka unaokuja wa fedha taratibu zikienda kama zilivyopanga fedha za fidia zitakuwa zinalipwa.

Mheshimiwa Spika, kwenye swali la pili ni kweli mradi huu ukikamilika utawafaa wananchi wa Mkoa wa Njombe, Wilaya ya Makete, lakini na Watanzania wengine wote kwa sababu ni mradi utakaopeleka umeme kwenye Gridi ya Taifa. Katika kipindi hiki ambacho umeme unakatika katika Serikali imeshafanya tathimini ya kujenga vituo vingine vya kupoza umeme kwenye maeneo mbalimbali na Makete ni eneo mojawapo ambalo limetizamwa kwa ajili ya kuboresha huduma ya umeme.