Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 9 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 150 2022-09-23

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA K.ny. MHE. FESTO R. SANGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Bwawa la Umeme la Mto Lumakali Wilayani Makete?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati naomba kujibu swali la Mheshimiwa Festo Richard Sanga, Mbunge wa Makete, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia TANESCO inaendelea na maandalizi ya utekelezaji wa Mradi wa Rumakali wa kuzalisha megawati 222 ulioko katika Wilaya ya Makete, Mkoani Njombe.

Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2022/2023 Serikali imetenga shilingi bilioni nane kwa ajili ya maandalizi ya awali ya mradi wa Rumakali. TANESCO imehuisha upembuzi yakinifu pamoja na kukamilisha nyaraka za zabuni za kumpata mkandarasi wa ujenzi. Aidha, uthamini wa mali za wananchi zinazopitiwa na mradi utakamilika mwezi Oktoba, 2022. Utekelezaji wa mradi huu unatarajiwa kuanza mwaka ujao.