Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza: - Je, ni vivutio gani vya utalii vimetambuliwa Wilayani Ukerewe na hatua zipi zimechukuliwa kuendeleza na kuvitangaza?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali ya nyongeza. Nitambue kazi kubwa inayofanywa na Wizara hii, pamoja na kutambua mikakati hii ambayo itasaidia kutangaza na kuviendeleza lakini bado sisi tulioko kwenye maeneo yale ikiwa ni pamoja na wataalam wa halmashauri hawana uelewa wa mikakati hii.

Sasa Mheshimiwa Waziri yupo tayari baada ya Bunge hili kuja Ukerewe ili kwa pamoja sasa wao na sisi pamoja na wataalam wa halmashauri tuweze kushirikishana mikakati hii ili iweze kuwa na tija?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; moja kati ya vivutio vilivyoko Ukerewe ni pamoja na beach ya Rubya ambapo pia kuna msitu ulio chini ya TFS. Lakini kwa kuwa Ukerewe tuna upungufu wa madawati karibu 6,000; Mheshimiwa Waziri kupitia CSR, TFS wako tayari kutusaidia kuondoa upungufu huo wa madawati 6,000? Nashukuru. (Makofi)

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Joseph Mkundi, Mbunge wa Ukerewe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, niko tayari kuambatana na Mbunge kwenda katika Kisiwa cha Ukerewe kuibua vivutio vilivyopo, lakini pia kuvitangaza. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini suala hili la pili la kuhusu beach ya Rubya ni kweli tuna hifadhi ya Rubya ambayo ni hifadhi ya msitu unaosimamiwa na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania na tumekuwa tukitoa CSR katika maeneo hayo na hivi karibuni tunakwenda kuzindua Kituo cha Polisi ambacho kimejengwa kutokana na hii Hifadhi ya Rubya. Kwa hiyo, nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge kwamba wajibu wa Serikali ni kuhakikisha kwamba maeneo yote ambayo tunayahifadhi wananchi walioko kwenye maeneo hayo wanafaidika na rasilimali iliyoko pale. Kwa hiyo, suala la madawati tutakwenda kulishughulikia na tutakwenda kuzungumza na wananchi ili waone umuhimu wa kuendeleza hifadhi hiyo.