Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 9 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 145 2022-09-23

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza: -

Je, ni vivutio gani vya utalii vimetambuliwa Wilayani Ukerewe na hatua zipi zimechukuliwa kuendeleza na kuvitangaza?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Michael Mkundi, Mbunge wa Ukerewe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Wizara katika kipindi cha mwaka 2020/2021 kwa kushirikiana na maafisa wa Mkoa wa Mwanza walitekeleza zoezi la kubaini na kuvitambua vivutio vya utalii vilivyopo katika Kisiwa cha Ukerewe. Vivutio hivyo ni pamoja na utalii wa ikolojia, utalii wa fukwe, utalii wa kiutamaduni na kihistoria.

Mheshimiwa Spika, Serikali imeweka mikakati ya kuvitangaza na kuviendeleza vivutio hivyo vya utalii kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa utalii hapa nchini. Sambamba na hilo Serikali inaendelea kuimarisha Ofisi ya Kanda ya Utalii iliyopo Jiji la Mwanza na kuanzisha Chuo cha Utalii cha Taifa katika Mkoa wa Mwanza kwa lengo la kusogeza huduma za Kanda ya Ziwa.