Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA K.n.y. MHE. JERRY W. SILAA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Pugu – Kifuru hadi Mbezi Mwisho kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri ya Serikali, na ni matarajio ya wananchi wa Jimbo la Ukonga ya kwamba barabara hizi zitatekelezwa kwa wakati kama Serikali ilivyoagiza.

Mheshimiwa Spika, swali dogo la nyongeza; kwa kuwa Serikali inao mpango na barabara nyingi zimeahidiwa ikiwemo barabara ya Msongola – Mbande yenye jumla ya kilometa 4.95. Ni lini Serikali inatoa ahadi ya kuanza kuijenga barabara hii kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Stanslaus Mabula, Mbunge wa Nyamagana, kwa niaba ya Mheshimiwa Jerry Silaa wa Ukonga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli barabara ya Msongola – Mbande hadi Mbagala (kilometa tano) sisi tunasema bado hazijajengwa kwa kiwango cha lami. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali imeanza mpango na tayari zabuni zimeshatangazwa. Tutaanza kuijenga kilometa mbili kwa mwaka huu wa fedha, ahsante. (Makofi)

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA K.n.y. MHE. JERRY W. SILAA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Pugu – Kifuru hadi Mbezi Mwisho kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana. na mimi ninapenda kujua ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara ya Mbalizi – Shigamba ambayo ni kiungo cha mikoa ya Mbeya na Songwe kupitia Ileje, na pia ni kiungo kwenda Nchi jirani ya Zambia?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Oran Njeza, Mbunge wa Mbeya Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya Mbalizi – Shigamba tayari zabuni zinaandaliwa kuitangaza kwa ajili ya kufanya feasibility study na usanifu wa kina ikiwa ni maandalizi kwa kuijenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami. Kwa hiyo mwaka huu tutahakikisha tunakamilisha feasibility study pamoja na usanifu wa kina, ahsante.

Name

Zuena Athumani Bushiri

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA K.n.y. MHE. JERRY W. SILAA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Pugu – Kifuru hadi Mbezi Mwisho kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. ZUENA A. BUSHIRI: Mheshimiwa Spika, ahsante na mimi kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara ya Mwembe – Mbaga – Mamba ambayo ni ahadi ya Mheshimiwa Hayati Rais Dkt. Magufuli?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya Mwembe – Mbaga ambayo iko Same ni barabara ambayo iko kwenye miinuko. Tulichokifanya kwa sasa, kabla ya kuanza kuijenga kwa kiwango cha lami ni kuainisha maeneo yote korofi na yenye miinuko ili tuweze kuyadhibiti na yaweze kupitika kwa mwaka wote, na baada ya hapo Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya kufanya feasibility study na usanifu wa kina ili kuijenga kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA K.n.y. MHE. JERRY W. SILAA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Pugu – Kifuru hadi Mbezi Mwisho kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, barabara ya Murushaka kwenda mpaka Murongo, ahadi ya Mheshimiwa Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, kilometa 50, imeshatangazwa muda mrefu lakini mpaka sasa hivi haijaanza ujenzi; nini tatizo lake?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Bilakwate, Mbunge wa Kyerwa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara haina shida, nataka tu nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kuwa tulishatangaza, mzabuni (mkandarasi) alishapatikana na tunategemea muda wowote ataoneshwa site ili aanze kutekeleza hiyo kazi, kilometa 50, kama zilivyoahidiwa na kama tunavyotegemea mkandarasi aanze kuifanya hiyo kazi. Ahsante.

Name

Agnesta Lambert Kaiza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA K.n.y. MHE. JERRY W. SILAA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Pugu – Kifuru hadi Mbezi Mwisho kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 5

MHE. AGNESTA L. KAIZA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili nami niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Jiji la Dodoma ni jiji kama yalivyo majiji mengine na hivyo linapaswa kuwa na hadhi zote za jiji. Sasa swali langu; ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara za mitaani kwa kiwango cha lami kwa mitaa yote ya Jiji hili la Dodoma?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Lambert kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nataka nimhakikishie kwamba jitihada kubwa sana zinafanyika kufanya kwamba barabara zote za Jiji la Dodoma zinafanyika. Tuna barabara za outer ring circuit na za inner ring circuit, lakini pia barabara zote ziko kwenye mpango kuhakikisha kwamba zinapanuliwa na kujengwa kwa kiwango cha lami ili kuhakikisha kwamba jiji linakuwa kweli na hadhi ya jiji, ahsante.

Name

Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA K.n.y. MHE. JERRY W. SILAA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Pugu – Kifuru hadi Mbezi Mwisho kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 6

MHE. BENAYA L. KAPINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona.

Ni lini Serikali itaimarisha, kuboresha na kudhibiti korongo kwenye Mlima wa Mawono, barabara ya Unyoni kuelekea Maguu wakati tunasubiri utekelezaji wa ujenzi wa lami kama Serikali ilivyoahidi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Benaya Kapinga, Mbunge wa Mbinga Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, korongo alilolisema naomba nitumie nafasi hii kumuagiza Meneja wa Mkoa wa Ruvuma aende akalitathmini na aone kazi ilivyo ili tuweze kupata gharama na tuweze kulikarabati ili isije ikaleta madhara ya kukata mawasiliano ili tuweze kulikarabati kabla ya kuanza kujenga hiyo barabara ama kuifanyia usanifu kwa maandalizi ya kuijenga kwa kiwango cha lami, ahsante.

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA K.n.y. MHE. JERRY W. SILAA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Pugu – Kifuru hadi Mbezi Mwisho kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 7

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, nina swali dogo la nyongeza kuhusiana na barabara inayotoka Mbagala kuelekea Temeke kutokea Kilungule - Mbagala kupitia Buza Kwa Mpalange; ni lini sasa itakamilisha ile lami? Kwa sababu wananchi wanapiga kelele sana. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dorothy Kilave, Mbunge wa Temeke, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara zetu nyingi za TANROADS na TARURA zinaingiliana. Lakini nitumie tu nafasi hii kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba azma ya Serikali ni kuzijenga barabara zote kwa kiwango cha lami na kwa kuwa barabara zimeshaanza kujengwa, tunamhakikishia kwamba Serikali itazikamilisha hizo barabara, ahsante.

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA K.n.y. MHE. JERRY W. SILAA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Pugu – Kifuru hadi Mbezi Mwisho kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 8

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi.

Je, ni lini Serikali itaanza kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Mlowo – Kamsamba kupitia Utambalila na Chitete ikiwa iko kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi mwaka 2025? Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Condester Sichalwe, Mbunge wa Momba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara Kamsamba – Utambalila – Chitete ni barabara ambayo ni sehemu ya barabara ya Mlowo – Utambalila – Kamsamba; barabara hizi ziko kwenye package moja. Kwa sababu tulishakamilisha usanifu, Serikali inaendelea kutafuta fedha ili kuijenga kwa kiwango cha lami, ahsante.

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA K.n.y. MHE. JERRY W. SILAA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Pugu – Kifuru hadi Mbezi Mwisho kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 9

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona.

Je, ni lini Serikali itaanza kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Buguni kuanzia Tengeru sokoni kupitia Kikwe hadi Mererani?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Pallangyo, Mbunge wa Arumeru Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja ni barabara ambayo ni muhimu sana kwa uchumi wa eneo hilo na Serikali ina mpango wa kuijenga kwa kiwango cha lami. Ikishakamilisha usanifu wa kina barabara hii tutaijenga kwa kiwango cha lami, ahsante.