Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 9 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 142 2022-09-23

Name

Jerry William Silaa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukonga

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA K.n.y. MHE. JERRY W. SILAA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Pugu – Kifuru hadi Mbezi Mwisho kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Jerry William Silaa, Mbunge wa Jimbo la Ukonga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika barabara ya Pugu – Kifuru – Mbezi Mwisho yenye urefu wa kilometa 12.7, sehemu ya kutoka Mbezi Mwisho hadi Kifuru (kilometa 6.7) imejengwa lami kwa njia mbili na sehemu ya kutoka Kifuru – Pugu Station (kilometa 6) ni barabara ya vumbi.

Mheshimiwa Spika, katika bajeti ya mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali imetenga fedha kwa ajili ya kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa sehemu ya Pugu Station hadi Kifuru (kilometa sita) kwa ajili ya ujenzi wa kiwango cha lami kwa njia nne na kwa sehemu ya Kifuru - Mbezi Mwisho (kilometa 6.7) kuipanua kutoka njia mbili kuwa njia nne. Zabuni kwa ajili ya kumpata mhandisi mshauri wa kufanya kazi hiyo zimetangazwa na zitafunguliwa tarehe 10 Oktoba, 2022. Baada ya kazi ya usanifu kukamilika Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi. Ahsante.