Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwanaisha Ng'anzi Ulenge

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE aliuliza: - Je, ni nini mkakati wa Serikali kuhusu mpango wa kukuza uchumi wa buluu kwa kuzingatia mazao yatokanayo na bahari?

Supplementary Question 1

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, pamoja na majibu mazuri ya Serikali naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mwani limekuwa ni zao ambalo linaingizia nchi nyingi fedha za kigeni na uzalishaji Tanzania kwa sasa ni tani 3,500 tu, lakini uhitaji uliopo kwa wanaotu-approach nchini kwetu ni tani zisizopungua 10,000. Swali langu ni kwamba ni upi mkakati wa Serikali wa kuongeza uzalishaji wa mwani nchini? Hilo ni swali la kwanza.

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; kutoka Tanga, ukanda huu wa mwambao wa bahari ya Hindi mpaka Mtwara, zaidi ya kilometa 1,084 kuna vikundi vya wanawake visivyopungua 8,000. Naomba kujua ni nini mkakati wa Serikali wa kuhakikisha masoko kwa wanawake hawa wanaozalisha mwani nchini na bei yenye tija?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa, Engineer Mwanaisha Ng’azi Ulunge, Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, la kwanza katika jibu la msingi nimeeleza juu ya mkakati wa Serikali wa kuweka shilingi bilioni 3.3 kwa ajili ya kuhakikisha kwamba tunakopesha vikundi vya akina mama kamba na kitu tunaita taitai, na kitu tunaita mbegu ili waweze kuongeza uzalishaji. Na hiyo tutagawa katika vikundi vyote pamoja na hivi vikundi alivyovitaja Mheshimiwa Ulenge. Kwa hiyo, hilo litasababisha kuongezeka kwa uzalishaji.

Mheshimiwa Spika, suala la bei na soko, nataka niwahakikishie kwamba kwa hali ilivyo na kwa uelekeo tunaouona, soko la mwani linazidi kukua siku hata siku na kwa msingi huo, tutakapokuwa na uzalishaji mkubwa, sasa uwezo wa kuweza kuliongoza soko katika bei utakuwa ni mkubwa, ni pamoja na kuweka mkakati wa bei elekezi ili zisishuke.

Mheshimiwa Spika, kama mwani aina ya spinosio uuzwe 800 kwenda juu, kama mwani wa aina ya kotonii uuzwe 2,000 kwenda juu. Huo ndiyo mkakati wetu tunaouelekea. Nashukuru.