Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 9 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 140 2022-09-23

Name

Mwanaisha Ng'anzi Ulenge

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE aliuliza: -

Je, ni nini mkakati wa Serikali kuhusu mpango wa kukuza uchumi wa buluu kwa kuzingatia mazao yatokanayo na bahari?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Engineer Mwanaisha Ng’anzi Ulenge, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika kukuza uchumi wa buluu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi chini ya uratibu wa Ofisi ya Makamu wa Rais na kwa kushirikiana na washirika wa maendeleo, mashirika ya kijamii, na sekta binafsi tunaandaa Mkakati wa Taifa wa Uchumi wa Buluu. Mazao ambayo yamepewa kipaumbele kwenye mkakati huo kwa upande wa baharini ni samaki aina ya dagaa, pweza, kambamiti, vibua, jodari, changudoa, zao la mwani, unenepeshaji wa kaa na ukuzaji wa lulu.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali imetenga jumla ya shilingi bilioni 11.51 ambazo zitatumika kununua boti za kisasa zenye engine, kifaa cha kutafutia samaki (GPS) na kasha la ubaridi lenye uwezo wa kubeba tani 1.5 kwa ajili ya kuwakopesha wavuvi. Pia jumla ya shilingi bilioni 20 zimetengwa ambapo kiasi cha shilingi bilioni 3.32 zitatumika kuwezesha pembejeo kwa ajili ya wakulima wa mwani katika ukanda wa bahari ya Hindi. Ahsante.