Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Edwin Enosy Swalle

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza: - Je, ni kwa nini Serikali isiteue Majaji wa muda mfupi (Acting Judges) ili kusikiliza kesi za mauaji zinazochukua muda mrefu Mahakamani?

Supplementary Question 1

MHE. EDWIN E. SWALLE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Ninayo maswali madogo mawili ya nyongeza; swali la kwanza kwa kuwa watuhumiwa wengi wanakaa muda mrefu mahabusu na kesi zao zinachelewa kwa sababu ya upelelezi. Ni lini Serikali italeta sheria Bungeni kuweka ukomo wa makosa ya jinai?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili kwa kuwa makosa mengi ambayo watu wanakaa muda mrefu kwenye mahabusu hayana dhamana; ni lini Serikali italeta Bungeni sheria ili kuruhusu makosa yote kuwa na dhamana?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, naomba kumjibu Mheshimiwa Edwin Enosy Swalle, Mbunge wa Lupembe swali lake la nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Bunge lako limekuwa linafanya marekebisho ya mara kwa mara ya sheria zetu hasa zile zinazohusu Penal Laws na Criminal Procedure Act ambayo kwa kumbukumbu nzuri Mheshimiwa Mbunge katika Bunge la mwezi Februari moja ya sheria inayohusu upelelezi ililetwa hapa katika mabadiliko madogo ya sheria na yako mabadiliko tuliyoyafanya ikiwemo kuruhusu sasa upeleleze ukamilike kwanza kabla kesi hazijapelekwa mahakamani.

Mheshimiwa Spika, lakini hata hivyo Katiba ya Jamhuri ya Muungano katika Ibara ya 13 katika issue za presumption of innocence nayo pia imesisitiza juu ya kuwepo kwa haki jinai ambazo zinataka mtu asiukumiwe kwanza isipokuwa kila mtu mbele ya sheria aonekane si mkosefu mpaka pale mahakama itakapodhibitisha jambo hilo.

Kwa hiyo, nataka nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge na kuhakikishia Bunge lako lote kwamba Serikali chini ya uongozi wa Rais wetu mama yetu Mama Samia Suluhu Hassan imeendelea kufanya mabadiliko ya sheria ili kukidhi haki ya jinai kama ambavyo umetaka ifanyiwe marekebisho.