Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 9 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 138 2022-09-23

Name

Edwin Enosy Swalle

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza: -

Je, ni kwa nini Serikali isiteue Majaji wa muda mfupi (Acting Judges) ili kusikiliza kesi za mauaji zinazochukua muda mrefu Mahakamani?

Name

Dr. Advocate Damas Daniel Ndumbaro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songea Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI K.n.y. WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria napenda kujibu swali la Mheshimiwa Edwin Enosy Swalle, Mbunge wa Lupembe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, uteuzi wa Majaji upo Kikatiba. Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania haina ibara inayotambua au kuruhusu uteuzi wa Majaji wa muda mfupi (Acting Judges). Aidha, Ibara ya 117(3) ya Katiba inatambua uwepo wa Mahakimu wenye mamlaka ya nyongeza ya kusikiliza baadhi ya mashauri ya Mahakama Kuu yakiwemo kesi za mauaji.