Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Primary Question

MHE. CHARLES J. MWIJAGE aliuliza: - Je, ni kwa nini Serikali isishirikishe sekta binafsi katika kilimo cha umwagiliaji ili kutimiza Ajenda 1030?

Supplementary Question 1

MHE. CHARLES J. MWIJAGE: Mheshimiwa Spika, naomba niulize maswali mawili madogo ya nyongeza: -

Mheshimiwa Spika, kutokana na kwamba, sasa Tanzania ni soko la chakula, naomba Serikali itueleze kasi ya Serikali katika kuwekeza kwenye umwagiliaji kwa kutumia sekta binafsi katika mito ambayo ina maji yasiyokauka, mito kama mabonde ya Kagera, basin ya Viktoria, Ruvuma na maziwa yetu? Hilo ni swali la kwanza.

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Katika maelezo ya hizo hekta 95,000 zinazozungumzwa naomba Serikali inihakikishie hekta 11,000 za Mto Ngono na zenyewe zimo?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Charles Mwijage, Mbunge wa Muleba Kaskazini, kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Spika, katika Jedwali la Sita katika Kitabu cha Bajeti iliyosomwa na Waziri wa Kilimo limeelezea mabonde 22 ambayo Serikali imeamua kuyafanyia upembuzi yakinifu na usanifu ili mwisho wa siku nchi yetu kuanzia Mashariki, Magharibi, Kusini na Kaskazini yote tufanye kilimo cha umwagiliaji. Nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge, mpaka hivi sasa ninavyozungumza tayari kazi hii imekamilika na tuko katika hatua za kuwapata Wakandarasi kwa ajili ya kufanya kazi hii.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, katika maeneo yote hayo mabonde yale makubwa, yaani kuanzia Bonde la Ziwa Viktoria, Malagarasi, Mto Manonga, Ifakara, Idete, Mto Songwe, Rufiji Basin Kwenda mpaka Mkoazi maeneo yote haya tutayagusa. Lengo letu ni kufanya kilimo cha umwagiliaji na mwisho wa siku tufikie malengo ambayo tumejiwekea. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili kuhusu Mto Ngono, kwenye hili la Mto Ngono nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge ambaye amekuwa akilisimamia sana jambo hili, katika yale mabonde 22 ambayo tunayafanyia upembuzi yakinifu na usanifu, Mto Ngono pia upo. Kwa hiyo, ekari zile 11,000 zitakuwepo kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge suala la Mto Ngono tumelichukulia katika umakini mkubwa sana. (Makofi/Kicheko)