Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 1 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 14 2022-09-13

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Primary Question

MHE. CHARLES J. MWIJAGE aliuliza: -

Je, ni kwa nini Serikali isishirikishe sekta binafsi katika kilimo cha umwagiliaji ili kutimiza Ajenda 1030?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Charles Mwijage, Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali katika utekelezaji wa miradi yake mbalimbali katika sekta ya kilimo, imeendelea kushirikiana bega kwa bega na sekta binafsi. Kwa muktadha huo, katika miradi ya umwagiliaji ambayo Serikali inatekeleza kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji imeendelea kuishirikisha sekta binafsi katika hatua mbalimbali za miradi hiyo ili kufikia malengo ya Agenda 10/30. Aidha, katika mwaka 2022/2023 Serikali imepanga kukarabati na kujenga miundombinu ya umwagiliaji katika eneo la hekta 95,000, ambapo jumla ya kandarasi 55 zimetolewa kwa sekta binafsi. Mpaka hivi sasa jumla ya mikataba 21 ya Wakandarasi imesainiwa na Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji.