Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itarejesha utoaji wa ruzuku ya pembejeo za dawa kwa wakulima wa kahawa?

Supplementary Question 1

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana nashukuru kwa majibu ya Serikali, lakini pamoja na majibu hayo ni ukweli usiofichika kwamba changamoto kubwa kwa uzalishaji wa kahawa ni hayo magonjwa uliyoyataja na mbegu zilizozalishwa bado hazijaweza kupambana na hayo magonjwa mia kwa mia.

Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kuanzisha mfuko wa maendeleo ya kahawa ili wakulima waweze kupata pesa za kununua pembejeo wapambane na magonjwa haya?

Mheshimiwa Spika, swali la pili je, kwa kuwa tumehamasisha sana uzalishaji wa kahawa, Serikali haioni pia ni muhimu kuanzisha programu za kuboresha mifereji ya asili ili wakulima waweze kupata maji ya kumwagilia kahawa zao? Ahsante.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Profesa Patrick Aloyce Ndakidemi, Mbunge wa Moshi Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, swali lake la kwanza sisi tunaona Mfuko wa Maendeleo ya Kilimo ambao tumeutamka katika bajeti yetu unatosha kwa ajili ya kushughulikia mazoa yote. Nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge ya kwamba zao la kahawa pia ni kati ya mazao ambayo yanashughulikiwa kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Kilimo na hivi sasa utaratibu ambao unaendelea ni kutenga kila shilingi mia moja kwenye zao la kahawa aina ya robusta na shilingi mia mbili kwa arabica kwa ajili ya kuchangia katika mfuko huu, kwa hiyo mwisho wa siku pia utakwenda kuhudumia zao la kahawa.

Mheshimiwa Spika, kuhusu mifereji, nakubaliana na wewe Profesa nami nimefika katika baadhi ya mashamba katioka Mkoa wa Kilimanjaro, hilo tumelichukua tunaendelea kulitekeleza, tutalifanyia kazi ili mwisho wa siku liweze kuleta tija kwa wakulima wetu. (Makofi)

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itarejesha utoaji wa ruzuku ya pembejeo za dawa kwa wakulima wa kahawa?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Swali langu ni fupi. Je, Serikali itatumia mkakati gani na ni lini itaanza kugawa hizo mbegu mnazosema tutagawiwa za ruzuku za miche ya kahawa kwa sababu muda unakwenda?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Kimei, Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, zoezi la ugawaji wa miche chotara linaendelea na tumeshagawa katika Mikoa ya Kagera, Mbeya, Songwe pamoja na Mkoa wa Kilimanjaro, pia hata Mheshimiwa Ndakidemi ni shahidi katika eneo lako miche hii imeshagawiwa. Zoezi ambalo tunaendea nalo ni kuhakikisha kwamba, tunazalisha kwa wingi ifikie miche Milioni 20 ili tuweze kubadilisha ile mibuni iliyokaa muda mrefu tui-replace na hii mipya ili kuondokana na changamoto ambayo wakulima wengi wanaipata.

Name

Kasalali Emmanuel Mageni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itarejesha utoaji wa ruzuku ya pembejeo za dawa kwa wakulima wa kahawa?

Supplementary Question 3

MHE. KASALALI E. MAGENI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Je, Serikali haioni kwamba, umefika wakati sasa wa kuwekeza kwenye uzalishaji wa mazao ya choroko na dengu kwa kutoa pembejeo na mafunzo kwa wakulima badala ya ambavyo sasa Serikali imewekeza zaidi kwenye kusimamia mauzo badala ya kusimamia uzalishaji? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Kasalali Mageni, Mbunge wa Sumve, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Kasalali kwa namna ambavyo amekuwa akiyasimamia mazao haya, hii ni hoja yake ambayo amekuwa akiisema mara kwa mara.

Mheshimiwa Spika, nataka nimhakikishie mbele ya Bunge hili ya kwamba, tutaendelea kuyapa kipaumbele mazao yote, katika maoni na ushauri ambao Mheshimiwa Mbunge ameusema tumeupokea tutakwenda kuufanyia kazi ili mwisho wa siku wakulima wa choroko na dengu pia walime kwa tija na masoko ya uhakika wayapate pia. (Makofi)

Name

Yahya Ally Mhata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Primary Question

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itarejesha utoaji wa ruzuku ya pembejeo za dawa kwa wakulima wa kahawa?

Supplementary Question 4

MHE. YAHYA A. MHATA: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa, msimu wa korosho unaanza mwezi wa Kumi. Je, Serikali haioni haja ya kuweka bei dira kwa zao la korosho kama ilivyo mazao mengine kama pamba?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, Yahya Mhata, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika kikao cha wadau tulichokifanya katika Manispaa ya Songea, katika kikao hiki mwongozo uliotolewa na ambao pia Serikali tunausimamia ni kwamba, utaratibu wa zamani wa bei ya korosho utaendelea ambapo ni utaratibu ule wa kulaza sanduku na baada ya hapo bei itakwenda kutangazwa ili mwisho wa siku wakulima waweze kuipata bei yao katika ufunguzi wa sanduku lile. Kwa hiyo, yale ambayo tulikubaliana na wadau na Waheshimiwa Wabunge pia walikuwepo ndiyo sehemu ya utekelezaji ambao Serikali tutausimamia.