Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Innocent Edward Kalogeris

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini

Primary Question

MHE. INNOCENT E. KALOGERIS aliuliza: - Je, ni lini ahadi ya ujenzi wa uwanja wa mpira Dodoma iliyotolewa na Mfalme wa Morocco itatekelezwa?

Supplementary Question 1

MHE. INNOCENT E. KALOGERIS: Mheshimiwa Spika, ni ukweli usiofichika kwamba ujenzi wa uwanja wa kisasa wa michezo na shughuli za Serikali kwa Makao Makuu ya Dodoma haukwepeki. (Makofi)

Je, Serikali pamoja na majibu ya kusema kutafuta wabia, wadau mbalimbali wa michezo, kwa nini Serikali isiwe na commitment kwamba mwakani katika bajeti tunatenga fedha ili ujenzi huo uanze, ukitilia maanani uwanja hauwezi kujengwa kwa mwaka mmoja?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Spika, nikushukuru, naomba kujibu swali moja la Mheshimiwa Innocent kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imekwisha kujipanga na ndio maana tumeshafanya upembuzi yakinifu kujua kwamba huu uwanja tunaujenga wapi, lakini kwa gharama gani. Huu uwanja unahitaji zaidi ya shilingi bilioni 420 na Serikali tuko kwenye hizo hatua pamoja na maongezi yanayoendelea lakini ndani ya Serikali tunaendelea kutafuta fedha.

Mheshimiwa Spika, nihakikishie Bunge hili tukufu huu uwanja pia ni ahadi ya Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020 na lazima tutaujenga.

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. INNOCENT E. KALOGERIS aliuliza: - Je, ni lini ahadi ya ujenzi wa uwanja wa mpira Dodoma iliyotolewa na Mfalme wa Morocco itatekelezwa?

Supplementary Question 2

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwanza kabisa nataka nimpongeze Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa kwa uzinduzi wa uwanja mzuri kule Ruangwa. Sambamba na pongezi hizo nataka niipongeze vilevile timu ya Namungo ambayo ilicheza na ikashinda vizuri sana kwenye ule uwanja wa nyumbani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali langu; je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza juhudi za wananchi katika kuhakikisha kwamba uwanja ule unakamilika?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Salma Rashid Kikwete kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, na sisi Serikali pia tumeendelea kumpongeza Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa kuonesha mfano katika suala zima la michezo na kuendeleza miundombinu ya michezo, lakini pia wenzetu wa Ruangwa pamoja na halmashauri yao.

Mheshimiwa Spika, sisi Serikali tumeendelea kuunga mkono jitihada za wadau mbalimbali kuhakikisha pia accessories za michezo kama nyasi bandia, lakini pia vifaa vya michezo kodi inapunguzwa. Sisi tutaendelea kushirikiana na halmashauri na watu binafsi kuhakikisha kwamba tunatengeneza mazingira rahisi ya uwekezaji katika michezo.

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. INNOCENT E. KALOGERIS aliuliza: - Je, ni lini ahadi ya ujenzi wa uwanja wa mpira Dodoma iliyotolewa na Mfalme wa Morocco itatekelezwa?

Supplementary Question 3

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwenye Bunge la Bajeti lililopita tulipitisha bajeti ya shilingi bilioni 10 kuweka nyasi bandia kwenye viwanja vya michezo nchini; je, Serikali imefikia hatua gani kwenye kuweka nyasi bandia kwenye viwanja vyetu kwa sababu ligi inaendelea na bado viwanja haviridhishi?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Spika, nikushukuru kwa nafasi kuweza kujibu swali la Mheshimiwa Festo Sanga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba katika bajeti iliyopita ya Bunge tulipitisha zaidi ya shilingi bilioni 10 kuhakikisha kwamba tunaboresha viwanja vya Arusha, Mwanza, Tanga, Dodoma, Mbeya na viwanja vyetu vikuu vya Mkapa ambavyo sasa vinatumika na vya Uhuru.

Mheshimiwa Spika, sisi kama Wizara tumeshaanza mchakato kuhakikisha kwamba mwaka huu wa fedha haupiti bila hizi fedha kutumika. Kwa hiyo, Wizara kupitia kitengo chetu cha manunuzi wameshaanza mchakato na tumeendelea kusisitiza kwamba jambo hili la kuboresha viwanja hivi iweze kuanza mapema ili hivi viwanja viweze kutumika. Ahsante.

WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri naomba nilithibitishie Bunge lako tukufu na Watanzania kwa ujumla kwamba viwanja hivi ambavyo Mheshimiwa Sanga amevizungumza havitawekwa tu nyasi bandia na nyasi za kawaida, tutakwenda kuweka viti vya kisasa kabisa. Pia viwanja hivi tunakwenda kuvitengeneza kwa namna ambavyo tunaweza kuvitumia kimataifa na mchakato huu wa ujenzi utaanza mwaka huu. (Makofi)