Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 1 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 11 2022-09-13

Name

Innocent Edward Kalogeris

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini

Primary Question

MHE. INNOCENT E. KALOGERIS aliuliza: -

Je, ni lini ahadi ya ujenzi wa uwanja wa mpira Dodoma iliyotolewa na Mfalme wa Morocco itatekelezwa?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, nikushukuru sana na kwa niaba ya Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo napenda kujibu swali la Mheshimiwa Innocent Edward Kalogeris, Mbunge wa Morogoro Kusini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imefuatilia utekelezaji wa ahadi ya ujenzi wa uwanja wa mpira Dodoma iliyotolewa na Mfalme wa Morocco. Mawasiliano kuhusu utekelezaji wa mradi huo baina ya Serikali ya Tanzania na Morocco bado yanaendelea. Vilevile katika kuhakikisha kwamba mradi huu unatekelezwa Serikali imedhamiria kutafuta fedha kutoka katika vyanzo mbalimbali vikiwemo sekta binafsi na wabia wa maendeleo.