Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mariam Madalu Nyoka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIAM M. NYOKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha jengo la hosteli ya madaktari watarajali katika Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma lililoanza kujengwa mwaka 2014/2015?

Supplementary Question 1

MHE. MARIAM M. NYOKA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, naomba niulize swali langu lingine la nyongeza.

Kwa kuwa mazingira ya nje ya majengo ya hospitali hii ya Mkoa wa Ruvuma sio rafiki hasa kwa watumishi na wagonjwa kwa kipindi cha mvua; je, Serikali ina mpango gani wa kuweka paving pamoja na kujenga mifereji ya maji ya mvua katika hospitali hii?

Name

Ummy Ally Mwalimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tanga Mjini

Answer

WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Mariam Madalu Nyoka kwa swali lake zuri, lakini kwa kufatilia maendeleo ya utoaji huduma katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Ruvuma.

Mheshimiwa Spika, nimwakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kipaumbele cha Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan ni kuboresha hospitali zote za rufaa za mikoa kwa kuwa ni kiungo muhimu cha utoaji huduma kati ya ngazi ya msingi na huduma za rufaa za juu. Kwa hiyo, tumepokea changamoto ya mazingira ya nje ambayo hayavutii na nikuahidi kwamba najua pia kuna suala la barabara tutawasiliana na TARURA ili pia kuweza kuweka lami katika barabara ambayo inaelekea kwenye hospitali ya rufaa ya mkoa.

Mheshimiwa Spika, suala la tent hilo ni jambo ambalo tutalifanyia kazi.

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIAM M. NYOKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha jengo la hosteli ya madaktari watarajali katika Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma lililoanza kujengwa mwaka 2014/2015?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Hospitali ya Mkoa wa Simiyu haina wodi za kulaza wagonjwa, wodi ya wanaume, wanawake na watoto; je, ni lini Serikali itajenga wodi hizo?

Name

Ummy Ally Mwalimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tanga Mjini

Answer

WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, nimshukuru sana Mheshimiwa Esther Midimu kwa swali lake la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwenye bajeti yetu ya 2022/2023 tumetenga fedha kwa ajili ya kuongeza wodi za kulaza wagonjwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu na baada ya Bunge mimi mwenyewe nitakwenda Simiyu pamoja na Mheshimiwa Esther Midimu ili kuhakikisha kwamba ujenzi unaanza haraka iwezekanavyo. (Makofi)