Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 1 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 10 2022-09-13

Name

Mariam Madalu Nyoka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIAM M. NYOKA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itakamilisha jengo la hosteli ya madaktari watarajali katika Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma lililoanza kujengwa mwaka 2014/2015?

Name

Ummy Ally Mwalimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tanga Mjini

Answer

WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mariam Madalu Nyoka, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imetenga kiasi cha shilingi bilioni moja katika mwaka wa fedha 2022/2023 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa jengo la hosteli ya madaktari watarajali (interns) katika Hospitali ya Mkoa Ruvuma.

Mheshimiwa Spika, ujenzi wa hosteli hii utaendelea mara tu fedha hizi zitakapokuwa zimetolewa na tunatarajia ujenzi huu utakamilika ifikapo Juni, 2023.