Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tauhida Cassian Gallos Nyimbo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TAUHIDA CASSIAN GALLOS aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kudhibiti ongezeko la uhalifu nchini?

Supplementary Question 1

MHE. TAUHIDA CASSIAN GALLOS: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa fursa hii kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa kumejitokeza suala la uhalifu ambao unafahamika kwa jina la panya road, je, Serikali ina mikakati ipi ya kuweza kuwaelimisha wananchi ili kuendelea kujikinga na suala hili la panya road?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, kwa kuwa uhalifu huu unafanyika Zaidi kwa silaha za jadi pamoja na silaha nzito. Serikali ina mkakati gani juu ya udhibiti wa silaha hizi?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Tauhida, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na utaratibu wa elimu kwa jamii kuhusu kukabiliana na uhalifu wa aina mbalimbali ikiwemo uhalifu ambao ameuzungumza Mheshimiwa Mbunge. Kwanza hivi karibuni tumeweka utaratibu wa kupeleka askari katika kila kata, kuna askari ambao walihitimu mafunzo ya kuupandishwa vyeo na hawa tumewatawanya katika kata zote nchi nzima kwa ajili ya kwenda kusaidia utaratibu na mifumo ya ulinzi shirikishi katika maeneo husika pamoja na utoaji elimu kwa wananchi.

Mheshimiwa Spika, kama hilo halitoshi hivi karibuni tumepata maelekezo kutoka kwa Amiri Jeshi Mkuu kwamba tuhakikishe tunakamilisha ununuzi wa magari ambayo yatakwenda moja katika wilaya na utaratibu wa kupeleka mafuta uende moja kwa moja wilayani kusaidia kuimarisha vitendea kazi kwa askari wetu walio karibu na wilaya na kata zetu kwa lengo la kuandaa mipango thabiti ya elimu kwa umma kuhusiana na ulinzi shirikishi pamoja na jitihada nzima za kushirikisha wananchi katika kusaidia vyombo vyetu vya usalama hususan Jeshi la Polisi katika kudhibiti uhalifu, si katika elimu tu hata kujipanga katika kudhibiti matukio ya kiuhalifu yasijitokeze.

Mheshimiwa Spika, nimjulishe Mheshimiwa Mbunge kwamba, baadaye Jeshi la Polisi watafanya mazungumzo na vyombo vya habari, watazungumza kutoa na kuainisha mkakati kabambe wa kupambana na waharifu ikiwemo Mkoa wa Dar es Salaam, hatua zilizofikia, mafanikio, changamoto, sababu na mipango ya kudhibiti jambo hilo lisiendelee kutokea zaidi. Kwa hiyo, nimwombe Mheshimiwa Mbunge pamoja na Waheshimiwa Wabunge wengine, wananchi wanaweza kupata ufafanuzi zaidi wa kina juu ya jambo hili hapo baadaye.

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. TAUHIDA CASSIAN GALLOS aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kudhibiti ongezeko la uhalifu nchini?

Supplementary Question 2

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona. Kumekuwepo na ongezeko kubwa la uhalifu na vitendo vya ukatili wa kijinsia kwenye mabasi yanayobeba wanafunzi wa shule za msingi na sekondari. Je, Serikali haioni ni wakati sahihi sasa kutoa maagizo kwamba mabasi haya yaendeshwe na madereva wanawake na makondakta wawe wanawake ili tunusuru ukatili wa kijinsia unaoendelea?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Saashisha Mafuwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, inawezekana ikawa ushauri wake ni moja kati ya mambo yanayoweza kusaidia, kwa hiyo tunauchukua. Hata hivyo, ziko na hatua zingine ambazo Serikali inazifanyia kazi, kwa pamoja tutajumuisha na ushauri wake ili tuweze kufanyia kazi ili matatizo kama haya yasijitokeze tena.

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. TAUHIDA CASSIAN GALLOS aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kudhibiti ongezeko la uhalifu nchini?

Supplementary Question 3

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Spika, asante sana kwa kuniona.

Swali langu ni kwamba je, Serikali ina mpango gani wa kujenga vituo vya polisi katika Tarafa za Kipatimu, Njinjo na Mandawa Wilayani Kilwa ili kudhibiti vitendo vya uhalifu katika Wilaya ya Kilwa?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Francis Ndulane, Mbunge wa Kilwa Kaskazini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nikiri juu ya changamoto ya upungufu wa vituo vya polisi katika kata za jimbo ambalo Mheshimiwa Mbunge ameeleza, lakini nizungumze kwa ujumla wake kwamba tuna upungufu wa vituo vya polisi tuna mpango wa kuongeza vituo vya polisi kwa miaka kumi zaidi ya mia tatu na hamsini na kitu ambavyo tunahitaji zaidi shilingi bilioni mia moja sitini na kitu.

Nataka nimwakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba mikakati ya kufanikisha mkakati huu wa ujenzi na Wabunge wengine ambao wana shida ya vituo vya polisi katika maeneo yao kwa miaka kumi, mwelekeo wa kuutekeleza mkakati huo katika kipindi kifupi sana upo katika hatua nzuri. Kwa hiyo, wakae mkao wa kula, lakini nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Wabunge wengine kwamba tuna mkakati kabambe na upo katika hatua nzuri ya kuukamilisha kabla ya muda uliopangwa ambao utatusaidia sana kupunguza changamoto za vituo vya polisi katika nchi hii.