Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 1 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 9 2022-09-13

Name

Tauhida Cassian Gallos Nyimbo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TAUHIDA CASSIAN GALLOS aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kudhibiti ongezeko la uhalifu nchini?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Tauhida Cassian Gallos, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Jeshi la Polisi inaendelea na mikakati yake ya kudhibiti vitendo vya uhalifu hapa nchini kwa kuimarisha doria, kufanya misako na operesheni mbalimbali dhidi ya uhalifu na wahalifu, pamoja kutoa elimu kwa jamii kutokujihusisha na vitendo vya uhalifu na kufuata sheria za nchi. Kushirikisha jamii kwenye ulinzi wa maeneo yao kupitia dhana ya ulinzi shirikishi. Pia Serikali imewapeleka wakaguzi wa polisi kwenye kata na shehia ili kushughulikia uhalifu kwa kushirikiana na wananchi.