Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA K.n.y. MHE. ALAUDIN H. SALIM aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali mpya ya Wilaya ya Ulanga?

Supplementary Question 1

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri au Wilaya katika Jimbo la Kilombero unaenda kwa kusuasua: Je, Serikali inawahakikishia nini wananchi wa Jimbo la Kilombero kwamba hospitali hiyo ya Halmashauri itakamilika?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Asenga ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, naomba nitoe maelekezo kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kilombero kuhakikisha anatumia fedha za Serikali zilizoletwa kwa ajili ya kujenga hospitali hiyo, na hospitali hiyo ikamilike kwa wakati kama mpango kazi ulivyo. Nasi Ofisi ya Rais, TAMISEMI, tutafuatilia kuona utekelezaji huo. Ahsante. (Makofi)

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA K.n.y. MHE. ALAUDIN H. SALIM aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali mpya ya Wilaya ya Ulanga?

Supplementary Question 2

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi ya swali la nyongeza. Hospitali ya Wilaya ya Kilwa maarufu kama Kinyonga iliyopo Kilwa Kivinje ni chakavu, lakini imeidhinishiwa fedha shilingi milioni 900: Lini Serikali itapeleka fedha hizo ili ukarabati ufanyike?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ally Kassinge, Mbunge wa Kilwa Kusini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba hospitali chakavu kama hospitali ya Wilaya ya Kilwa maarufu “Kinyonga”, imetengewa Shilingi milioni 900 na katika mwaka huu wa fedha Serikali inaendelea kutafuta fedha ili tupeleke katika hospitali hiyo kwa ajili ya ukarabati. Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. David Mathayo David

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Same Magharibi

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA K.n.y. MHE. ALAUDIN H. SALIM aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali mpya ya Wilaya ya Ulanga?

Supplementary Question 3

MHE. MATHAYO D. MATHAYO: Mheshimiwa Spika, Kata ya Vudee na Kata ya Mshewa katika Jimbo la Same Magharibi, ni miongoni mwa Kata za kujengewa vituo vya afya vya kimkakati: Je, ni lini Serikali itajenga vituo vya afya katika Kata ya Vudee na Kata ya Mshewa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mathayo David Mathayo, Mbunge wa Same Magharibi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mbunge kwamba Serikali iliainisha kata zote za kimkakati kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya na tutakwenda kujenga vituo vya afya hivyo kwa awamu ikiwemo kata hizi za kimkakati katika Jimbo la Same Magharibi. Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Ezra John Chiwelesa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA K.n.y. MHE. ALAUDIN H. SALIM aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali mpya ya Wilaya ya Ulanga?

Supplementary Question 4

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Wilaya ya Biharamulo, tuna ujenzi wa hospitali ya Wilaya pale, lakini ujenzi ule umekwama kwa muda mrefu kwa sababu ya pesa iliyorudishwa Shilingi milioni 204. Hii fedha nimeisema mbele ya Rais akiwa Biharamulo tarehe 8 Juni, na TAMISEMI wakaahidi kwamba wanakwenda kuifuatilia: Ni lini sasa fedha hii italetwa ili tuweze kukamilisha kwa sababu kila kitu kiko tayari pale isipokuwa fedha hii? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Engineer Ezra Chiwelesa, Mbunge wa Jimbo la Biharamulo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli Mheshimiwa Mbunge amefuatilia sana suala ya fedha hizi na ameshauliza hapa. Tulikubaliana na Hazina kwa maana ya Wizara ya Fedha, fedha zile ziweze kurejeshwa kwa ajili ya ujenzi wa hospitali hiyo. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutafuatilia sisi na Wizara ya Fedha, tuhakikishe fedha zinakwenda kwa ajili ya ujenzi wa hospitali hiyo. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA K.n.y. MHE. ALAUDIN H. SALIM aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali mpya ya Wilaya ya Ulanga?

Supplementary Question 5

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Halmashauri ya Mji wa Bunda, imeanza ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri kwenye Kata ya Bunda Store, na Serikali ilitenga Shilingi milioni 500: Kuna mkakati gani wa kutenga fedha kila mwaka wa fedha ili ile hospitali iweze kukamilika haraka? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ester Bulaya, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, dhamira ya Serikali ni kuendelea kutenga fedha kila mwaka wa fedha, ndiyo maana tulipeleka Shilingi milioni 500 na kila mwaka wa fedha tutatenga Shilingi milioni 500 au zaidi kuhakikisha Hospitali ya Mji wa Bunda pia inakamilika. Ahsante.