Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

George Natany Malima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. GEORGE N. MALIMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafanya ukarabati wa Hospitali ya Wilaya ya Mpwapwa?

Supplementary Question 1

MHE. GEORGE N. MALIMA: Mheshimiwa Spika, pamoja na jibu zuri la Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza ni kwamba, pamoja na uchakavu wa hospitali hii, lakini hatuna gari la wagonjwa: Je, ni lini Serikali italeta gari la kubebea wagonjwa (ambulance)?

Mheshimiwa Spika, swali la pili: Ni lini Waziri atafanya ziara katika hospitali hii ya Wilaya ya Mpwapwa ili ajionee hali halisi ya hospitali ile? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa George Natany Malima, Mbunge wa Jimbo la Mpwapwa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba mwaka huu wa fedha atapata gari la wagonjwa kwa ajili ya Hospitali ya Wilaya katika Halmashauri ya Mpwapwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pili, nilifanya ziara mwezi wa Nne mwaka huu katika Hospitali ya Mpwapwa, lakini nipo tayari kuongozana na Mheshimiwa Mbunge kwenda kufanya ziara tena kuona namna ya kuboresha huduma pale. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GEORGE N. MALIMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafanya ukarabati wa Hospitali ya Wilaya ya Mpwapwa?

Supplementary Question 2

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Nini mpango wa Serikali kupeleka vifaa tiba kwenye zahanati zilizokamilishwa kwa nguvu za wananchi hasa katika Vijiji vya Mundarara, Loremeta, Gelai Lumbwa, vilivyopo katika Wilaya ya Logindo, Mkoa wa Arusha? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Catherine Magige, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika mwaka huu wa fedha Serikali imetenga Shilingi bilioni 69.95 kwa ajili ya kupeleka vifaa tiba katika vituo 530 zikiwemo hizi zahanati ambazo zimejengwa kwa nguvu za wananchi. Ahsante. (Makofi)