Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Eng. Ezra John Chiwelesa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA aliuliza: - Je, ni lini kiasi cha shilingi milioni 204 zilizorejeshwa Hazina mwaka wa fedha 2019/2020 zitatolewa kwa ajili ya ujenzi wa majengo mawili ya Hospitali ya Wilaya ya Biharamulo?

Supplementary Question 1

MHE ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi, lakini kwa idhini yako nichukue nafasi hii kuwashukuru sana Watanzania ambao wamenifanya ni-trend wiki hii na kauli mbiu yangu ya kuchumba chima. (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa ni mara yangu ya pili sasa ninaulizia hii pesa ya shilingi milioni 204 ikizingatiwa kwamba kuna baadhi ya suppliers ambao tayari walikwisha- supply vifaa na leo hii ni miezi 18 wanaidai Serikali. Ninaomba kupata kauli thabiti ya Serikali, ni lini pesa hii itapelekwa ili tumalizane na hili tatizo kwa sababu wanadai zaidi ya miezi 18 baadhi ya watu pale?

Pili, kwa kuwa sasa wananchi wangu wa Biharamulo ambao ni wafanyabiashara wamelazimika kuingia kwenye hali y kuikopesha Serikali bila makubaliano ya mikopo.

Je, Serikali ipo tayari kuwalipa na riba hawa watu ambao wame-supply vifaa na leo wanatakiwa walipwe pesa yao? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, ahsante; kwa ruhusa yako naomba nijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Engineer Ezra Chiwelesa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kabla ya kujibu naomba nimpongeze sana kwa jinsi ambavyo anajitahidi kufuatilia wananchi wa Jimbo hilo kwa maendeleo na maslahi ya Wilaya yake.

Mheshimiwa Spika, suala la ulipaji madeni Serikali siku zote ipo katika harakati za kuhakikisha kwamba imelipa madeni ya wadai wote. Zipo taratibu ambazo zinafuatwa za kujiridhisha na kuhakiki madeni hayo ili baadae tuweze kulipa kwa utaratibu.

Mheshimiwa Spika, kwa wale ndugu zetu ambao walishatumikia miezi 18 lakini fedha hiyo haijapatikana, tumeshatoa mpaka kufikia Januari mwaka huu tumeshatoa shilingi milioni mia tatu kuja katika Jimbo lako la Halmashauri ya Biharamulo. Katika fedha hiyo mnaweza mkatenga fedha maalum kupunguza taratibu deni la wananchi ambao walitumikia Jimbo hilo. Ahsante sana. (Makofi)