Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 14 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 169 2022-02-18

Name

Eng. Ezra John Chiwelesa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA aliuliza: -

Je, ni lini kiasi cha shilingi milioni 204 zilizorejeshwa Hazina mwaka wa fedha 2019/2020 zitatolewa kwa ajili ya ujenzi wa majengo mawili ya Hospitali ya Wilaya ya Biharamulo?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante; kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Engineer Ezra John Chiwelesa, Mbunge wa Biharamulo Magharibi, kama ifuatavyo: -

Mshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2019/2020, kiasi cha shilingi milioni 500 kilitengwa na kutolewa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Biharamulo. Hadi kufikia tarehe 30 Juni, 2020 kiasi cha shilingi milioni 204 kilikuwa hakijatumika, hivyo kilirejeshwa kwenye Mfuko Mkuu wa Serikali kwa mujibu wa Sheria ya Bajeti kifungu namba 29(1).

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, nia ya Serikali ni kuhakikisha kuwa wananchi wanapata huduma za afya karibu na maeneo yao. Hivyo kutokana na umuhimu wa mradi huu, katika mwaka wa fedha 2020/2021 Serikali ilitenga na kutoa shilingi bilioni moja kwa ajili ya uendelezaji wa ujenzi wa hospitali hii. Vilevile katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali imetenga kiasi cha shilingi milioni 676.6; shilingi milioni 300 kwa ajili ya uendelezaji wa ujenzi na shilingi milioni 376.6 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba.

Mheshimiwa Spika, hivyo Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo inahimizwa kuomba fedha hizo mapema ili kuendelea na ukamilishaji wa ujenzi wa Hospitali hiyo ya Wilaya ikiwemo majengo mawili aliyoyataja Mheshimiwa Mbunge. Ahsante. (Makofi)