Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Taska Restituta Mbogo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya kutoka Mpanda kwenda Karema kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. TASKA R. MBOGO: Mheshimiwa Spika, ahsante; ninayo maswali mawili ya nyongeza.

Kwa kuwa barabara ya kutoka Mpanda kwenda Karema upembuzi yakinifu unakamilika mwezi wa Aprili na kwa kuwa barabara hiyo ni muhimu, inakwenda kwenye Bandari ya Karema ambako Serikali imewekeza shilingi bilioni 47 na kwa kuwa asilimia 81 ya ujenzi wa bandari imekamilika; na kwa kuwa bandari hiyo...

SPIKA: Mheshimiwa Taska Mbogo uliza swali.

MHE. TASKA R. MBOGO: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa bandari hiyo inakwenda kupokea mzigo kutoka nchi za SADC. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kwamba barabara hiyo inajengwa na kukamilika kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa barabara iliyopo sasa hivi ina changamoto kwenye maeneo ya Kaseganyama, Kandilankulukulu na Nkungwi haipitiki kipindi cha masika. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuongeza bajeti ili barabara hiyo ipitike kipindi cha masika? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Taska Restituta Mbogo, Mbunge wa Viti Maalum Katavi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama alivyosema na kama nilivyosema kwenye jibu langu la msingi kutokana na umuhimu wa barabara hii ambavyo kama alivyosema, Serikali imewekeza zaidi ya shilingi bilioni 47 kukamilisha bandari ambayo ipo asilimia 79; ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba hii barabara itakapokamilika kufanyiwa usanifu mwezi Aprili zitatafutwa fedha haraka ili iweze kujengwa kwa kiwango cha lami tukitambua kwamba ndio litakuwa lango kubwa la bidhaa zetu kwenda DRC. Ahsante. (Makofi)

Name

Francis Isack Mtinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya kutoka Mpanda kwenda Karema kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. FRANCIS I. MTINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi; kwa kuwa barabara ya Iguguno kupitia Nduguti mpaka daraja la Sibiti inaunganisha Mkoa wa Singida na Simiyu na inapita makao makuu ya Wilaya.

Je, Serikali haioni haja ya kujenga kipande cha kilometa 42 kutoka Iguguno mpaka makao makuu ya Wilaya kwa mtindo wa build and design? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Francis Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ina mpango wa kujenga barabara hii lakini daraja alilolisema tunajenga daraja la msingi na hili daraja ambalo amelisema, liko kwenye mpango wa kufanyiwa usanifu ili liweze kujengwa kwa kiwango cha zege.

Kwa hiyo, naomba baada ya hapa tukutane na Mheshimiwa Mbunge ili tuweze kuelekezana zaidi jinsi kazi hii itakavyofanyika. Ahsante. (Makofi)

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya kutoka Mpanda kwenda Karema kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Spika, ahsante; tatizo lililopo Mpanda ni sawa sawa na tatizo lililopo kwenye Wilaya ya Kahama, Halmashauri ya Msalala Jimbo la Msalala; barabara inayotoka Bulyanhulu kwenda Kahama; barabara hii imekuwa ni mbovu sana mwaka jana imetengewa shilingi bilioni 3...

SPIKA: Uliza swali Mheshimiwa.

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Spika, swali langu ni lini sasa Serikali itaanza ujenzi wa barabara hii inayotoka Bulyanhulu kwenda Kahama kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Iddi Kassim Mbunge wa Msalala kama ifutavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya Bulyanhulu – Segesi – Kahama ni sehemu tu ya barabara inayoanzia Geita – Bukoli
– Bulyanhulu – Segesi - Kahama na kama alivyosema barabara hii imetengewa fedha, lakini niliwahi kujibu kwenye jibu la msingi swali lililopita kwamba kuna mazungumzo ambayo wenzetu wa Barrick wameonesha utayari wa kuijenga barabara hii kwa kiwango cha lami na mazungumzo bado yanaendelea. Kama watakwama basi Serikali itachukua hatua ya kuijenga barabara hiyo. Ahsante. (Makofi)

Name

Selemani Jumanne Zedi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukene

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya kutoka Mpanda kwenda Karema kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. SELEMANI J. ZEDI: Mheshimiwa Spika, ahsante; barabara ya kutoka Tabora – Mambari – Bukene – Itobo – Kahama ilishafanyiwa, usanifu wa kina na ilitengewa fedha kwa ajili ya kujengwa kwa kiwango cha lami.

Je, ni sababu zipi zinafanya ujenzi huu usianze licha ya kuwa imeshatengewa fedha? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Selemani Zedi Mbunge wa Bukene kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli barabara ya Tabora – Mambari – Ntobwa – Nzega imeshafanyiwa usanifu wa kina na ipo kwenye mpango wa kujengwa kwa kiwango cha lami. Kwa hiyo, nimuhakikishie Mbunge kwamba Serikali inatafuta fedha na itakapopatikana hiyo fedha, tutaanza kwa sababu tayari ipo kwenye mpango na ipo kwenye bajeti. Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Josephat Mathias Gwajima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kawe

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya kutoka Mpanda kwenda Karema kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 5

MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza; barabara ya Bunju B, Msitu wa Mabwepande mpaka Mbezi Mwisho ilipandishwa daraja kutoka TARURA kuingizwa TANROADS na Mheshimiwa Rais aliahidi kwamba itajengwa kwa kiwango cha lami. (Makofi)

Je, ni lini sasa Serikali itajenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Josephat Gwajima kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kama alivyosema barabara hii ilikuwa inahudumiwa na TARURA na kwa kuwa imepandishwa daraja naomba nimuombe Mheshimiwa Mbunge kuwa katika kipindi hiki cha bajeti tuweze kuhakikisha kwamba barabara hii imeingia kwenye mpango ili tunapoanza utekelezaji wa bajeti inayofuata barabara hii iweze kujengwa kwa kiwango cha lami kama Mheshimiwa Rais alipoipandisha na kuhakikisha kwamba inajengwa kwa kiwango cha lami. Ahsante. (Makofi)

Name

Furaha Ntengo Matondo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya kutoka Mpanda kwenda Karema kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 6

MHE. FURAHA N. MATONDO: Mheshimiwa Spika, ninashukuru sana kwa kunipa nafasi.

Je, ni lini barabara ya Airport kwenda Nyanguge yenye urefu wa kilometa 46 kupita Kayenze itawekewa lami kwa kuwa barabara hiyo ipo kwenye Ilani ya Uuchaguzi? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Furaha Matondo, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mwanza, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli barabara ya Airport – Nyanguge ni kama by pass kwa upande wa magari yanayokwenda njia ya Musoma na ni kweli ipo kwenye mpango na Serikali inatafuta fedha. Tumewasiliana sana na Mheshimiwa Angelina Mabula ambaye ni Mbunge mwenyewe akiwa anaifuatilia hii barabara.

Mheshimiwa Spika, ninataka nimhakikishie kwamba bado ipo kwenye mpango na itajengwa kwa kiwango cha lami. Ahsante. (Makofi)