Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 14 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 168 2022-02-18

Name

Taska Restituta Mbogo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya kutoka Mpanda kwenda Karema kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante; kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Taska Restituta Mbogo, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Barabara ya Mpanda – Kagwira - Karema yenye urefu wa kilometa 122 ambapo kipande cha Mpanda – Kagwira chenye urefu wa kilomita 10, ni sehemu ya barabara Kuu na sehemu ya Kagirwa – Karema yenye jumla ya urefu wa kilometa 112 ni barabara ya Mkoa.

Mheshimiwa Spika, mnamo mwezi Machi, 2021 Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) ilisaini Mkataba na Kampuni ya M/s Crown Tech. Consultant Ltd. kwa ajili ya kufanya Upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara ya Kagwira – Karema yenye urefu wa kilometa 112 kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami na kazi hii inategemea kukamilika mwezi Aprili, 2022.

Mheshimiwa Spika, mara baada ya kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kukamilika na gharama za ujenzi kujulikana, Serikali itaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuijenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami. Ahsante. (Makofi)