Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Venant Daud Protas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kumalizia maboma yaliyojengwa kwa nguvu za wananchi kwa ajili ya elimu, afya na polisi?

Supplementary Question 1

MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Spika, ahsante, kwanza mimi nimpongeza Mheshimiwa Waziri kwa majibu mazuri na tunakiri kabisa kwamba wameleta fedha.

Nina maswali mawili ya nyongeza; la kwanza, mwaka 2017 Mheshimiwa Waziri Mkuu alikuja katika Kata ya Goweko, Kijiji cha Imalakaseko kulikuwa na wodi ambayo walianzisha wananchi, aliahidi ataleta shilingi milioni 80 tangu mwaka 2017 mpaka leo hazijafika? Lakini vilevile aliyekuwa Waziri wa TAMISEMI Selemani Jaffo mwaka 2019 alikuja katika Kata ya Igalula wodi ipo pale wananchi walianzisha aliahidi ataleta fedha mpaka leo, halikadhalika na kata zingine.

Mheshimiwa Spika, nataka nijue nini kauli ya Serikali kulinda ahadi za viongozi endapo wanatoa ahadi na hazitekelezeki kwa wakati?

Swali langu la pili ni mkakati gani Serikali sasa itatoa kumaliza maboma yote ili kuwatia nguvu na moyo wananchi ambao wamejitoa kuisaidia Serikali? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Daud Protas Venant, Mbunge wa Jimbo la Igalula kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kauli ya Serikali ni kwamba ahadi zote za Viongozi wetu wa Kitaifa ni lazima zitatekelezwa na nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ahadi hii ya milioni 80 ya Mheshimiwa Waziri Mkuu tutapeleka fedha hizi kabla ya mwisho wa mwaka wa fedha 2021/2022. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini kuhusu na suala la mkakati wa umaliziwaji wa maboma katika jibu langu la msingi nimeeleza namna ambavyo Serikali kwanza imepeleka fedha nyingi kwenye maboma, lakini kuyatambua maboma yote zaidi ya 1700. Lakini tatu tunatafuta fedha na kupeleka kwa awamu kwa ajili ya kukamilisha maboma hayo.

Mheshimiwa spika, kwa hiyo nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Waheshimiwa Wabunge wote kwamba mkakati wa Serikali uko thabiti na tutaendelea kuyakamilisha maboma hayo kupitia mapato ya ndani na mapato ya Serikali Kuu. Ahsante sana. (Makofi)