Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 14 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 161 2022-02-18

Name

Venant Daud Protas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kumalizia maboma yaliyojengwa kwa nguvu za wananchi kwa ajili ya elimu, afya na polisi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Venant Daud Protas, Mbunge wa Jimbo la Igalula kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua uwepo wa maboma 1,715 ya zahanti na vituo vya afya yaliyoanzishwa kwa nguvu za wananchi ambayo yanahitaji jumla ya shilingi bilioni 98.7 kwa ajili ya ukamilishaji wake. Aidha, katika sekta ya elimu kuna jumla ya maboma 12,101 ambayo yanahitaji jumla ya shilingi bilioni 183.5 kwa ajili ya ukamilishaji wake.

Mheshimiwa Spika, katika Bajeti ya mwaka 2021/2022 Serikali imetenga shilingi bilioni 43.8 kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma ya zahanati na vituo vya afya ambapo hadi kufikia Desemba, 2021 shilingi bilioni 29.5 zimepelekwa kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma hayo. Aidha, katika mwaka wa fedha 2021/22 Serikali imetenga shilingi bilioni 79 kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma ya madarasa na maabara ambapo fedha hizo tayari zimekwishapelekwa.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali imetenga shilingi bilioni mbili kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa vituo vya polisi 63 vilivyoanzishwa na wananchi kwa ajili ya kuimarisha huduma za usalama wa raia na mali zao katika maeneo yao ambapo hadi kufikia Desemba, 2021 shilingi bilioni 1.85 zimekwishatolewa sawa na asilimia 85. Mkakati wa Serikali ni kuendelea kutenga fedha kwa awamu. Ahsante.