Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza: - Je, Serikali inatoa kauli gani juu ya udanganyifu mkubwa kwenye mikataba ya Ushuru wa kampuni za Simu na wenye maeneo pale panapojengwa minara ya simu kiasi cha kusababisha ushuru kwenda kwa watu wasiohusika?

Supplementary Question 1

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwanza nitoe shukrani kwa majibu mazuri ya Serikali juu ya swali langu, lakini nina maswali mawili ya nyongeza: -

Mheshimiwa Spika, kwani upo udanganyifu uliofanywa katika Kijiji cha Kibutuka na aliyekuwa mfanyakazi wa Tigo, alienda pale akadanganya wanakijiji kwamba, anahitaji eneo la kujenga mnara, baadaye wanakijiji walimpa bure wakitumia mukhtasari ule yule sasa hivi anekuwa ndio mnufaika wa kodi ya mnara ule badala ya kuwa wanakijiji waliopo katika kijiji kile.

Je, Serikali ina mkakati gani au ina kauli gani juu ya utapeli wa huyu mtumishi wa tiGO ambaye yeye anajifanya kwamba, ndio mmiliki wa lile eneo wakati aliliomba apewe bure?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; pamoja na kwamba, Vijiji vya Ndapata, Ndunyungu, Makata, Mtawatawa, Kipelele, Makinda na Nambinda havina mawasiliano ya kutosha. Nini mkakati wa Serikali wa kutuwashia ile minara ambayo tayari imeshawashwa kwenye baadhi ya vijiji hapa nchini?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali ya Mheshimiwa Zuberi Mohamed Kuchauka, Mbunge wa Liwale, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika kipengele cha kwanza. Ni kweli kabisa changamoto ya udanganyifu uliojitokeza tunaifahamu, lakini tayari suala hili lilikuwa limeshafika mahakamani na lilikuwa limeshatolewa maamuzi.

Mheshimiwa Spika, tunafahamu pia migogoro ya ardhi inapotokea kwa Sheria Na.2 ya Mwaka 2002, tunafahamu kabisa kwamba, hili linahusisha Wizara ya Ardhi moja kwa moja, lakini nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwa changamoto hii ambayo imejitokeza tutashirikiana na wenzetu wa Wizara ya Ardhi, ili tuweze kujua namna gani tutatatua changamoto hii ambayo imejitokeza katika eneo husika.

Mheshimiwa Spika, vilevile swali la pili ni kuhusu minara ambayo haijawashwa. Ni kweli kabisa katika maeneo ya Jimbo la Liwale, kwanza kabisa labda tuseme kwamba, Serikali imefanya uwekezaji mkubwa sana katika ujenzi wa minara ndani ya nchi yetu, likiwepo Jimbo la Liwale. Ni takribani bilioni 19.56 imewekezwa katika minara 161 ambapo tunatarajia katika kipindi cha miezi miwili mitatu minara hii ambayo tayari imeshasimama itahakikisha kwamba, itakuwa imeshawashwa.

Mheshimiwa Spika, Serikali pia imefanya uwekezaji mwingine wa minara 127 ambayo iko katika hatua za civil works. Katika kipindi cha miezi miwili mitatu, tunaamini kabisa kwamba, minara hii itakapokamilika, naamini maeneo mengi yatakuwa yamepata ufumbuzi wa changamoto hizi za mawasiliano, likiwepo Jimbo la Mheshimiwa Kuchauka ambalo ni Liwale. Nakushukuru sana.