Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itasambaza maji katika Vijiji vya Mwanjoro, Jinamo, Mbushi na Witamihya Wilayani Meatu baada ya ujenzi wa Bwawa la Mwanjoro kukamilika?

Supplementary Question 1

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Spika, ninaomba nimshukuru Mheshimiwa Rais na Wizara kwa kuidhinisha na kutekeleza mradi wa dharura katika Mji wa Mwaluzi siku si chache wananchi wataanza kunufaika na Mto semu.

Mheshimiwa Spika, kutokana na changamoto zilizoainishwa katika majibu ya Serikali ninamuomba Mheshimiwa Naibu Waziri afike Jimbo la Meatu katika Bwawa hilo ilia one hizo adhan a kuchukua hatua za haraka ili kunusuru bwawa hilo lililogharimu Shilingi Bilioni 1.8 bila kunufaisha wananchi.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa mradi huu ulitekelezwa na Wizara, RUASA Wilaya kwa mwaka uliotajwa tayari mipango mingine imewekwa. Je, ukarabati huu utafanywa kwa ngazi ya Mkoa au ngazi ya Wizara? Ninakushukuru. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, awali ya yote ninapenda kupokea pongezi na kwa hakika tuna kila sababu ya kuendelea kumuombea Mheshimiwa Rais Mama Samia Suluhu Hassan kwa namna ambavyo ameitendea haki hii Wizara ya Maji. Tumeendelea kupata fedha na ndiyo maana tunaona kila kona miradi ya maji inaendelea kutekelezwa.

Mheshimiwa Spika, kufika Meatu ni moja ya taratibu zangu za kazi, naomba nikupe taarifa Mheshimiwa Mbunge pamoja na Wabunge wote wanaotoka Mkoa wa Simiyu ratiba yangu ni kuanzia tarehe 25 mwezi huu kuwa Simiyu hivyo tutafika maeneo haya yote korofi ili kuona tunafanya kazi kwa pamoja.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na ukarabati tutafanya kwa kushirikiana na watendaji wetu ambao wapo katika Mkoa ule na Wizara hatuna pa kukwepea ni lazima tuwajibike katika hilo. (Makofi)

Name

Salome Wycliffe Makamba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itasambaza maji katika Vijiji vya Mwanjoro, Jinamo, Mbushi na Witamihya Wilayani Meatu baada ya ujenzi wa Bwawa la Mwanjoro kukamilika?

Supplementary Question 2

MHE. SALOME W. MAKAMBA: Mheshimiwa Spika, Jimbo la Shinyanga Mjini katika Kata za pembeni, Kata ya Chibe, Mwalili, Old Shinyanga, Kizumbi na Mwawaza kuna shida kubwa sana ya maji, watu wanakunywa maji ya kwenye madimbwi.

Ni nini mpango wa Serikali kupeleka mtandao wa maji kwenye Kata hizi kwa sababu hata sasa ukiwafuata Mamlaka ya Maji wanasema hawana fedha kwa ajili ya kupeleka maji safi na salama. Nini mpango wa Serikali wa kuhakikisha kwamba wanapeleka fedha na kupeleka maji katika Kata hizo za pembezoni.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Salome Makamba, maeneo ya Shinyanga Mjini ni kweli imekuwa ni moja ya maeneo ambayo yamekuwa changamoto ya maji, lakini Wizara hapa tulipo chini ya uongozi thabiti wa Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan siyo Wizara ya wananchi kunywa maji kwenye madimbwi.

Mheshimiwa Spika, hili tayari tumeendelea kulifanyia kazi na maeneo haya yote ambayo bado yana changamoto, Wizara tutaleta fedha, tutasimamia kuhakikisha kwamba Majimbo yote, maji yatapatikana ili kuona wananchi wanapata maji safi bombani na ya kutosha. (Makofi)

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itasambaza maji katika Vijiji vya Mwanjoro, Jinamo, Mbushi na Witamihya Wilayani Meatu baada ya ujenzi wa Bwawa la Mwanjoro kukamilika?

Supplementary Question 3

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, ninataka kujua ni lini Serikali itakamilisha mradi mkubwa wa maji wa Mwanga, Same, Korogwe ili kusaidia usambazaji wa maji kwenye vijiji vya Kata ya Mtomazi na Mkumbara katika Wilaya ya Korogwe? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, huu ni mradi mkubwa ambao umeshachukua muda mrefu lakini Wizara tunaendelea kutekeleza tunaamini ndani ya muda wa usanifu tunakwenda kukamilisha wa phase hii ambayo tupo. Mheshimiwa Mbunge tuendelee kushirikiana na hongera kwa kuendelea kufuatilia mradi huu muhimu. (Makofi)