Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ally Anyigulile Jumbe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Primary Question

MHE. ALLY A. J. M. JUMBE aliuliza: - Je, Serikali inachukua hatua gani ili kuhakikisha kwamba maji yote yaliyopo ardhini yanabaki salama kwa kuwa tone moja la oil (vilainishi) huharibu lita 600 za maji yaliyoko ardhini?

Supplementary Question 1

MHE. ALLY A. J. M. JUMBE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwa kuwa Mto Kiwira unapita maene mengi sana ya Wilaya ya Kyela ikiwemo Vijiji vya Lema, Mwalisi, mpaka Bujonde. Na kwa kuwa mto huo umelalamikiwa na wananchi wa maeneo hayo kuwa na uchafuzi mkubwa ambapo inafikia hatua mto unanuka na unakuwa na rangi ya damu.

Je, ni lini Serikali itaunda Tume Maalum kufanya utafiti wa nini kinasababisha maji hayo yawe machafu?

Mheshimiwa Spika, mbili, kwa kuwa wananchi wengi wa eneo hilo baada ya kukosa maji ya Ngana wanatumia kwa ajili ya kunywa na kuoga. Je, ni lini Serikali sasa itaanza ujenzi wa mradi wa Ngana?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, kwanza ninapenda kumpongeza Mheshimiwa Ally amekuwa mfuatiliaji mzuri, amekuwa anakwenda zaidi ya uhitaji wa kupata maji yakiwa bombani lakini pia amekuwa akizingatia suala la usalama.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na bonde hili maji haya yanapochafuka, Mto Kiwira ni Mto ambao tunautumia kwa miradi mingi, naomba kutumia Bunge lako Tukufu kuagiza Bonde husika lifanye kazi kadri ambavyo inatakiwa kisheria. Vilevile Wizara tutaendelea kusimamia. Tayari Mheshimiwa Waziri amekuwa akitoa maagizo kadhaa kwa Mabonde yote kuhakikisha shughuli za maji kuwa salama yafanye usimamizi unaotakiwa.

Mheshimiwa Spika, kuhusu swali lake la pili la lini ujenzi wa Ngana utaanza, kwa furaha kubwa ninapenda kukuarifu Mheshimiwa Mbunge kwamba mradi huu tayari tumeshatangaza na hivi karibuni kabla yam waka huu wa fedha kuisha tutapata Mkandarasi na lazima kasi zije zianze kwa kasi kwa sababu tunafahamu umuhimu wake kulingana na jiografia ya eneo hilo. (Makofi)

Name

Michael Mwita Kembaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Mjini

Primary Question

MHE. ALLY A. J. M. JUMBE aliuliza: - Je, Serikali inachukua hatua gani ili kuhakikisha kwamba maji yote yaliyopo ardhini yanabaki salama kwa kuwa tone moja la oil (vilainishi) huharibu lita 600 za maji yaliyoko ardhini?

Supplementary Question 2

MHE. MICHAEL M. KEMBAKI: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, katika Mji wetu wa Tarime tunategemea chanzo kimoja kikuu cha maji ya Bonde la Ndurumo, lakini kumetokea baadhi ya watu kuanzisha plant za kuchenjua dhahabu kandokando ya chanzo hiki.

Je, Serikali inatuhakikishiaje watu wa Tarime kwamba maji tunayotumia yapo salama? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, maji yote ambayo yanafika kwa mlaji wa mwisho kwa maana ya mwananchi ni maji salama ambayo tayari Wizara kupitia Idara ya Maabara inakuwa imeshafanya kazi yake, hivyo ninapenda kuwatoa hofu wananchi wote wanaoishi kandokando ya wachimbaji kwamba maji yanafanyiwa kazi katika maabara.

Name

Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. ALLY A. J. M. JUMBE aliuliza: - Je, Serikali inachukua hatua gani ili kuhakikisha kwamba maji yote yaliyopo ardhini yanabaki salama kwa kuwa tone moja la oil (vilainishi) huharibu lita 600 za maji yaliyoko ardhini?

Supplementary Question 3

MHE. BENAYA L. KAPINGA: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru. Mradi wa maji wa Litembo, Mahenge kutokea Mwogelo, mwaka jana niliuliza swali hapa na nikapewa majibu mazuri na Mheshimiwa kwamba tayari fedha imetengwa na mradi unaanza kujengwa. Kwa bahati mbaya mradi huu unatoa maji Litembo tu.

Je, ni lini maji yatatoka Mahenge na Langandondo? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ni kweli anachokiongea Mheshimiwa Mbunge lakini Mheshimiwa Mbunge unafahamu kwa namna ambavyo tumekuwa tukiwasiliana tumeweza kufanya kazi sasa Litembo inapata maji. Kwa hiyo, maeneo haya ya Mahenge tayari tunapeleka Mkandarasi ambaye ataanza kazi hivi karibuni na kuona kwamba maeneo yote haya mawili yaliyobaki nayo yanakwenda kunufaika na maji bombani.

Mheshimiwa Spika, ninaomba Mheshimiwa Mbunge tuendelee kushirikiana kwa pamoja kama ambavyo umekuwa ukifanya. (Makofi)