Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 13 Water and Irrigation Wizara ya Maji 156 2022-02-17

Name

Ally Anyigulile Jumbe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Primary Question

MHE. ALLY A. J. M. JUMBE aliuliza: -

Je, Serikali inachukua hatua gani ili kuhakikisha kwamba maji yote yaliyopo ardhini yanabaki salama kwa kuwa tone moja la oil (vilainishi) huharibu lita 600 za maji yaliyoko ardhini?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ally Anyigulile Jumbe Mlaghali, Mbunge wa Kyela kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Sheria ya Usimamizi wa Rasilimali za Maji Na. 11 ya mMwaka 2009 na Sheria ya Mazingira Na. 20 ya Mwaka 2004 kwa pamoja zinasisitiza uhifadhi, utunzaji na usimamizi wa vyanzo vya maji. Maji chini ya ardhi ni rasilimali ambayo inalindwa dhidi ya uchafuzi wa aina zote hii ni pamoja na oil. Hii ni kutokana na kuwa maji chini ya ardhi yakishaharibiwa ubora wake ni vigumu na ni gharama kubwa kuyasafisha ili yaweze kutumika kwa shughuli za maendeleo.

Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Bodi za Maji za Mabonde inaendelea na jukumu la kutambua vyanzo vya maji juu ya ardhi na chini ya ardhi, kuweka mipaka na kutangaza katika Gazeti la Serikali ili yalindwe kisheria. Hivyo, maeneo tengefu ambayo yametangazwa ni Saba (7) ambapo Sita (6) ambayo yalitangazwa mwaka 2016 yapo Bodi ya Maji Bonde la Ziwa Rukwa maeneo ya Chokaa, Kidole, Kiswaga, Matundasi A, Matundasi B na Mkola katika Wilaya ya Chunya Mkoa wa Mbeya na eneo moja Makutupora Mkoani Dodoma katika Bonde la Wami-Ruvu lilitangazwa mwaka 2012.

Mheshimiwa Spika, vilevile, maeneo Hamsini na Nne (54) katika Bodi ya Maji Bonde la Rufiji (16), Ziwa Tanganyika (3), Pangani (7), Wami/Ruvu (5) Ruvuma na Pwani ya Kusini (13), Ziwa Nyasa (8) na Ziwa Victoria (1), Bonde la Kati (1) yamewekewa mipaka ili yatangazwe mwaka huu 2022.

Mheshimiwa Spika, katika kuimarisha utekelezaji wa Mipango ya Uhifadhi wa Vyanzo vya maji, Wizara ya Maji inatekeleza kazi ya kuainisha miamba yenye maji (Aquifer Mapping) katika Mabonde manne ambayo ni Bonde la Kati, Pangani, Wami/Ruvu na Rufiji.

Mheshimiwa Spika, kazi ya kutathmini maeneo yenye maji chini ya ardhi imekamilika na hatua inayofuata ni kuchimba visima ili kupata takwimu za wingi na ubora wa maji katika maeneo hayo. Baada ya hatua hii, itaandaliwa ramani ili kutangaza maeneo hayo katika Gazeti la Serikali ili yalindwe kisheria na yaweze kutumika kulingana na mahitaji ya shughuli za maendeleo.