Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwanaisha Ng'anzi Ulenge

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE aliuliza: - Je, nini kauli ya Serikali kutokana na mkanganyiko uliotokea kuhusu fidia katika barabara ya Tanga – Pangani?

Supplementary Question 1

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa zoezi la fidia lilianza mwaka, 2012 mpaka 2013 kama sikosei na verification imekuja kufanyika mwaka 2015; na mpaka wananchi kulipwa, wamelipwa mwaka 2021 ambayo ni takribani miaka tisa: -

Je, Serikali haioni haja wale ambao hawakulipwa kwa mujibu wa Sheria yetu ya Barabara ya 2007, ukiwaacha pembeni kulingana na sheria ya awali ya masharti ya ADB kufutwa machozi kwa kuzingatia kwamba wamekaa miaka tisa bila kufanya maendeleo yoyote? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; kwa kuwa malalamiko ya kupotezewa muda mwingi wananchi yapo Tanzania nzima kwenye suala zima la kulipwa fidia: -

Je, ni lini Serikali itaileta Sheria ya Barabara ya Mwaka, 2007 Act (No. 13) tukirekebishe kifungu Na. 16 ili kuweze kuongeza muda wa kuwalipa fidia wananchi? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Eng. Mwanaisha Ng’anzi Ulenge, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Tanga. Kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kuwapigania haki wananchi wa Mkoa wa Tanga ambao anawatetea.

Mheshimiwa Spika, swali lake la kwanza, naomba nimjulishe Mheshimiwa Mbunge kwamba katika fidia za wananchi hawa wapo ambao waliridhika na wamechukua fidia, lakini wale ambao hawakuridhika, suala hili walilifikisha Mahakamani. Kwa hiyo, naomba nisiitolee maelezo zaidi.

Mheshimiwa Spika, swali la pili kuhusu mMarekebisho ya sheria, naomba niseme tumelichukua na tutakwenda kulifanyia kazi. Ahsante. (Makofi)

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE aliuliza: - Je, nini kauli ya Serikali kutokana na mkanganyiko uliotokea kuhusu fidia katika barabara ya Tanga – Pangani?

Supplementary Question 2

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwa kuwa barabara ya kutoka Nyigu kwenda Mgololo ambako ndiko kuna kiwanda kikubwa cha karatasi ambao ni uwekezaji mkubwa sana; na ni barabara ya uchumi ambayo imekuwa ikiwasaidia sana wananchi wa eneo hilo: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha barabara hiyo inajengwa kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Deo Sanga, Mbunge wa Makambako, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli barabara hii ni muhimu sana na mbao nyingi tunazoziona zinapita kwenye hii barabara. Naomba tu nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba suala hili amekuja ofisini kama yeye kuliongelea.

Mheshimiwa Spika, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba hizi ni barabara za kimkakati. Kwa hiyo, namwomba yeye pamoja na wananchi wavute subira kwamba, kulingana na umuhimu wake na jinsi inavyoliingizia Taifa fedha nyingi, basi itakuwepo kwenye mpango ili iweze kujengwa kwa kiwango cha lami. Ahsante. (Makofi)

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE aliuliza: - Je, nini kauli ya Serikali kutokana na mkanganyiko uliotokea kuhusu fidia katika barabara ya Tanga – Pangani?

Supplementary Question 3

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Ujenzi wa barabara ya Mgakorongo kwenda Murongo tathmini imefanyika na wananchi wamekuwa wakisubiri fidia kwa muda mrefu, kiasi kwamba wanashawishika kufanya maendeleo: -

Je, ni lini fidia zitaanza kutoka ili wananchi waweze kuhamia sehemu nyingine waendelee na maisha yao? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Anatropia, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Wabunge wanaohusika na barabara hii ya kuanzia Omugakarongo, Kigarama hadi Murongo; hii barabara ipo kwenye maandalizi ya kutangazwa zabuni. Barabara hii kabla haijaanzwa tutahakikisha kwamba wananchi hawa kipaumbele ni kuwalipa fidia. Kwa hiyo, kabla hatujaanza kujenga, wananchi kwanza watalipwa fidia na ujenzi wa hiyo barabara utaanza. Ahsante. (Makofi)

Name

Eric James Shigongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Primary Question

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE aliuliza: - Je, nini kauli ya Serikali kutokana na mkanganyiko uliotokea kuhusu fidia katika barabara ya Tanga – Pangani?

Supplementary Question 4

MHE. ERIC J. SHIGONGO: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa changamoto wanayoipata wananchi wa maeneo ya Tanga na Pangani ni sawa sawa na matatizo waliyonayo wananchi wa Buchosa ambao ahadi ya Serikali ilikuwa ni kujenga barabara kutoka Sengerema, Nyehunge mpaka Kahunda, lakini wananchi wale wamesimamisha shughuli zao wakisubiri fidia na ujenzi uanze: -

Je, Mheshimiwa Waziri anaweza kuwaambia wananchi wa Buchosa ni lini fidia zitalipwa na lini barabara itaanza kujengwa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Eric Shigongo, Mbunge wa Buchosa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara anayoitaja ya Sengerema – Nyehunge hadi Kahunda yenye kilomita zisizopungua 82 ipo kwenye maandalizi. Kama nilivyosema kwa barabara iliyopita, ni kati ya barabara ambazo zinategemea kuanzwa kujengwa kwa kiwango cha lami kuanzia mwaka huu wa fedha. Kabla ya kuanza ujenzi sheria inatuambia tuwalipe kwanza fidia. Kwa hiyo, mara tutakapoanza kutangaza ujenzi huo, basi na wananchi watapatiwa fidia kwanza. Ahsante. (Makofi)