Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza kiwango cha mkopo wa 10% kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu?

Supplementary Question 1

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Spika, ahsante, ninashukuru kwa majibu ya Serikali, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali langu la kwanza ni, kwa sababu wanawake au makundi haya kwa sasa hivi yanapata mkopo kwa kiwango kidogo sana kiasi kwamba mkopo huo hauwasaidii.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza kiwango hicho kutoka milioni mbili na laki tano kwa kila kundi mpaka milioni kumi ili waweze kufanya vizuri kwenye biashara zao?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; Serikali sasa ina mpango gani wa kuwajengea mafunzo na uwezo kabla makundi haya hayajapewa mkopo?

Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Bupe Nelson Mwakang’ata, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, makundi haya ambayo ni ya wajasiriamali wanawake, vijana na watu wenye ulemavu yanakopesha asilimia 10, kwa maana ya 4:4:2, lakini kiwango cha ukopeshaji hakijaainishwa, inategemea aina ya shughuli ya ujasiriamali, si kila kikundi kinakopesha milioni mbili na laki tano. Kila kikundi kinakopeshwa kuliangana na uhitaji wa biashara yao, lakini pia uwezo wa kurejesha fedha zile baada ya kukopeshwa.

Mheshimiwa Spika, na Serikali imetoa tamko kwamba tunahitaji kuona vikundi vya wajasiriamali wanakopeshwa fedha zenye kiwango ambacho kinaleta tija ya kuwawezesha kutoka hatua moja kwenda hatua nyingine badala ya kutoa fedha kidogokidogo ambazo kwanza haziwawezeshi kiuchumi, lakini pili inakuwa ni changamoto kuzirejeshwa. Kwa hiyo, maelekezo haya yametolewa, na Mheshimiwa Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan ameelekeza na sisi Ofisi ya Rais TAMISEMI tunalitekeleza.

Mheshimiwa Spika, na nichukue nafasi hii kutoa maelekezo kwa halmashauri zote kuhakikisha kwamba wanatoa fedha yenye tija badala ya kutoa fedha kidogo kidogo kwa vikundi vya wajasirimali.

Mheshimiwa Spika, mpango wa mafunzo umewekwa vizuri. Maafisa Maendeleo ya Jamii katika hamashauri zetu wanawajibika kwanza kuwajengea uwezo kwa maana ya mafunzo pamoja na kuwatembelea na kuhakikisha kwamba wanafanya biashara zao, na zoezi hili ni endelevu. Ahsante.

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza kiwango cha mkopo wa 10% kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu?

Supplementary Question 2

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Waliokuwa Bungeni kabla yetu waliona busara kwamba asilimia 10 iende kwa wanawake, na baadae sasa makundi yale yalivyobainika ikaonekana ile ile asilimia 10 igawanywe kwa walemavu na vijana.

Je, Serikali haioni sasa ni wakati mwafaka wanawake wakabaki na ile asilimia 10 na yale makundi mengine yakapatiwa asilimia yao?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Shally Raymond, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Sheria ya Mikopo ya Ujasiriamali iliyopitishwa na Bunge hili mwaka 2019 inaelekeza asilimia 10 kwa ajili ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu. Ni kweli kwamba tulianza na asilimia 10 kwa wanawake, lakini baada ya tathimini ya makundi yenye uhitaji wa kujengewa uwezo wa ujasiriamali yaliongezeka makundi ya vijana pamoja na makundi ya watu wenye ulemavu.

Mheshimiwa Spika, makundi haya yote ni muhimu kujengewa uwezo katika jamii yetu. Hata hivyo tunachukua wazo lake kuendelea kufanya tathmini. Lakini kabla hatujafikia hatua hiyo tunafanya tathmini ya ufanisi, changamoto na mafanikio ya hii asilimia 10, kwa maana ya 4:4:2, na baada ya hapo tutaona maeneo gani tuboreshe ili tuweze ku-accommodate mawazo ya Waheshimiwa Wabunge. Ahsante sana.

Name

Anastazia James Wambura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza kiwango cha mkopo wa 10% kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu?

Supplementary Question 3

MHE. ANASTAZIA J. WAMBURA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kuna zile fedha za marejesho za miaka iliyopita ambazo huwa zinajeshwa ambazo inaonekana kwamba kila halmashauri inakuwa na utaratibu wake.

Mheshimiwa Spika, nini kauli ya Serikali kuhusiana na hizi fedha zinazorejeshwa ambazo zingeweza kuongeza kiasi cha wanaokopa wakapata fedha nyingi zaidi? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la Mheshimia Wambura, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, maelekezo ya fedha za marejesho ya asilimia 10 zimefunguliwa akaunti zake mahsusi, kwa hiyo wajasiriamali wanaporejesha fedha zile zinatakiwa kuingizwa kwenye akaunti mahsusi ya marejesho ya mikopo ya asilimia 10. Akaunti ile ni revolving fund, maana yake baada ya kurejeshwa zinatakiwa kuendelea kuwakopesha vikundi vya wajasiriamali. Kwa hiyo, matarajio ya Serikali ni kwamba akaunti zile kila baada ya mwaka wa fedha zitakuwa zinaendelea kuongezeka na kutakuwa na fedha za kutosha zaidi.

Mheshimiwa Spika, naomba nitumie nafasi hii kumhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali ilitoa maelekezo, na hakuna halmashauri inayotakiwa kwenda kinyume na maelekezo haya. Nitoe wito kwamba halmashauri zote ni lazima zihakikishe kwamba akaunti za marejesho zinafanya kazi, na fedha zile zikirejeshwa ziendelee kukopesha wajasiriamali wengine.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana.