Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 13 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 149 2022-02-17

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza kiwango cha mkopo wa 10% kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bupe Nelson Mwakang’ata, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ilianzisha utaratibu wa kutoa mikopo inayotokana na asilimia 10 ya mapato ya ndani ya halmashauri kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu ili kusaidia makundi haya kuendasha shughuli zao za ujasiriamali na kujiongezea kipato.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa Serikali haijaweka mpango wa kuongeza asilimia ya mikopo hiyo. Aidha, tathmini ya kina inafanyika ili kubaini mafanikio na changamoto zilizopo ili hatua stahiki zichukuliwe katika kuboresha mikopo hiyo.