Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itanunua Magari ya kisasa ya Zimamoto ili kunusuru maisha ya raia na mali zao?

Supplementary Question 1

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwanza niseme nasikitishwa na majibu ya Serikali: -

Mheshimiwa Naibu Spika, sote tunafahamu jinsi Taifa letu linavyokumbwa na majanga mbalimbali ya moto, kama kuungua kwa masoko, shhule, nyumba binafsi na hata kwenye biashara mbalimbali kama hoteli na vinginevyo, ambayo inasababisha hasara kwa mali za raia, lakini hata uhai wao.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa, magari ya kisasa, on average, ni kuanzia milioni 500 na kuendelea. Na bajeti ya Serikali imeonesha kutenga bilioni mbili tu kwa maana ya kwamba, watanunua walao magari manne tu tena hayo ni ya wastani. Ni kwanini sasa Serikali isione umuhimu wa kutenga fedha kwa udharura, ili waweze kununua magari walao mawili katika kila halmashauri, kama ambavyo wanafanya kwenye magari ya washawasha? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili, sote tumeshuhudia wakati wa chaguzi ambazo zinafanyika kila baada ya miaka mitano kwenye majimbo yetu kunakuja magari ya washawasha zaidi ya mawili matatu, ambayo gari moja la washawasha ni takribani milioni 500, kama ilivyo kwa gharama za gari la zimamoto. Je, kipaumbele cha Serikali ni kipi kati ya kulinda mali ya raia na uhai wao dhidi ya kudhibiti wapinzani wakati wa uchaguzi? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Esther Nicholas Matiko, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema kwenye jibu langu la msingi. Serikali inatenga fedha mwaka huu, imetenga mwaka jana bilioni mbili na nusu, mwaka huu imetenga bilioni mbili. Tutaendelea kutenga fedha hizo au zaidi kutegemea upatikanaji wa fedha ili kuimarisha jeshi hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia nikumbushe. Jeshi la Zimamoto na Uokoaji halifanyi kazi peke yake, hushirikisha majeshi mengine na vituo vingine kama viwanja vya ndege, bandari na kadhalika.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili, tunathamini mali na wananchi wetu kwa hiyo, mfano anaoutoa wa washawasha hauna uhusiano wa moja kwa moja na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji.nashukuru sana. (Makofi)

Name

Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itanunua Magari ya kisasa ya Zimamoto ili kunusuru maisha ya raia na mali zao?

Supplementary Question 2

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa nafasi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda ilikuwa na gari zuri la zimamoto, gari ambalo lilikuwa ni la kisasa. Kwa bahati mbaya lilipata ajali mwaka 2015, toka Serikali imelichukua kwa ajili ya matengezo, gari hilo halijaweza kurejeshwa Mpanda. Swali langu, ni lini Serikali itaturejeshea gari hilo zuri na la kisasa?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Mbunge, la nyongeza, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, tuna interest na Tanga kutokana na miradi mingi mliyonayo ya kiuchumi ikiwemo bandari na bomba la mafuta linalopita pale. Tutafuatilia baada ya Bunge hili kuona kwamba, matengenezo ya gari hilo yanakamilika lirejeshwe Tanga kwa ajili ya kuendelea kutoa huduma kwa wananchi. Ahsante sana.

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itanunua Magari ya kisasa ya Zimamoto ili kunusuru maisha ya raia na mali zao?

Supplementary Question 3

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali: -

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na uchakavu wa Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Hai, lakini Wilaya ya Hai ina watumishi 149, hakuna nyumba hata moja ya watumishi hawa, kiasi kwamba, OCD, OC-CID na Mkuu wa Kituo cha Polisi Wilaya ya Hai anakaa mbali sana kwa hiyo, wanashindwa kutoa huduma pale. Ni lini sasa Serikali itajenga walao hata nyumba moja tu ya Mkuu wa Kituo Wilaya ya Hai?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Saashisha Mafuwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni nia ya Serikali kuweka mazingira bora ya utendaji wa kazi wa vyombo vyetu vya ulinzi, hasa vya usalama, ikiwemo Polisi, Zimamoto, Magereza,
n.k. Kama nilivyosema katika jibu nililotoa juzi, tunaendelea kutenga fedha na mwaka huu zipo fedha zimetengwa kwa ajili hiyo. Lengo ni kuhakikisha kwamba, maeneo yote ambayo hayana nyumba yanapewa kipaumbele ikiwemo wilaya yako ya Hai. Ahsante sana

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itanunua Magari ya kisasa ya Zimamoto ili kunusuru maisha ya raia na mali zao?

Supplementary Question 4

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, swali langu mimi ni, kule Temeke Kata ya Sandali, kuna jengo kubwa sana ambalo mmelijenga la zimamoto, lakini mpaka sasa halijamaliziwa wala hakuna vifaa vyovyote ambavyo vimeingizwa kwa ajili ya zimamoto.

Je, ni lini sasa vifaa hivi pamoja na jingo lile litamalizika kwa ajili ye Serikali yetu?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kilave, Mbunge wa Temeke, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nalifahamu amelizungumzia suala hilo la eneo la Mchicha majuzi, tutalipa kipaumbele kwa interest ya watu wa Dar es Salaam, uchumi wao na shughuli nyingi za kiviwanda zinazotekelezwa ili kuwawezesha Fire kutimiza majukumu yao kwa ufanisi.