Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 12 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 141 2022-02-16

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itanunua Magari ya kisasa ya Zimamoto ili kunusuru maisha ya raia na mali zao?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Esther Nicholas Matiko, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeandaa mpango mkakati wa kuimarisha huduma za zimamoto na uokoaji nchini kwa kuimarisha na kuongeza vifaa vya kisasa vya utendaji kazi katika Jeshi la Zimamoto na Uokoaji. Vifaa hivi vya kisasa vitaenda sambamba na upelekaji wa huduma ya zimamoto na uokoaji katika wilaya zote ambazo hazina huduma hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Jeshi la Zimamoto na Uokoaji nchini imetenga bajeti ya maendeleo ya shilingi bilioni 2 katika mwaka wa fedha 2021/2022 kwa ajili ya kununua magari mapya ya kisasa ya zima moto. Lengo la ununuzi wa magari haya ni kuongeza ufanisi kwenye shughuli za kuokoa maisha na mali za wananchi, pindi patokeapo ajali za moto na nyingine. Taratibu zote za ununuzi zikikamilika, magari ya kuzima moto yatapelekwa mikoa isiyokuwa na huduma ya zimamoto na uokoaji. Serikali itaendelea kutenga fedha kila mwaka ili kuliwezesha vitendea kazi stahiki Jeshi la Zimamoto na Uokoaji.