Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza kuwasaidia Wachimbaji wadogo wa madini katika Mji wa Njombe kama inavyofanya kwenye maeneo mengine?

Supplementary Question 1

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza: -

Mheshimiwa Naibu Spika, swali kwanza, kwa vile wananchi wachimbaji wa Njombe, kupitia chama chao cha wachimbaji kinaitwa WANANJO, walishafikisha kilio kwa Mheshimiwa Waziri na Waziri akatoa maelekezo kwa Katibu Mkuu kwamba, watafutiwe na watengewe maeneo kama inavyofanyika maeneo mengine katika nchi yetu. Na kwa vile mchakato huo ulishafanyika na RMO alishafikisha hayo mapendekezo ya maeneo wizarani.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali, ni lini sasa wananchi hawa watapewa hayo maeneo ambayo tayari yameshatambuliwa kwamba, ni muhimu kwa uchimbaji wa wachimbaji wadogo wa Njombe?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa, ameongelea kuwasaidia kwa kupitia training mbalimbali pamoja na mikopo. Wananchi, wachimbaji wale, hawana Habari na hiyo training ni kalenda ambayo Wizara wamejipangia. Naomba tupate uhakika na wao wasikie, ni lini mafunzo haya yatafanyika katika Mkoa wa Njombe? (Makofi)

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali madogo ya nyongeza ya Mheshimiwa Deodatus Mwanyika, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa swali lake la kwanza ambapo anataka kujua kwamba, wachimbaji wadogo walioahidiwa maeneo ya kuchimba makaa ya mawe, na ninafahamu ni katika eneo la Ludewa, ni lini watapewa hayo maeneo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumhakikishia kwamba, taasisi yetu husika ambayo ni Tume ya Madini walishakwenda kupima maeneo hayo na mpaka sasa wameshapata kilometa za mraba 10.33 ambazo zinatosha kutoa leseni za wachimbaji wadogo 120. Na wanaendelea kutafuta maeneo ya ziada ili kuwapatia wachimbaji wote wadogo maeneo ya kuchimba kulingana na maombi yao.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa swali lake la pili, napenda kumhakikishia Mbunge, Ndugu yangu Mwanyika ambaye nampongeza sana kwa jinsi anavyowapambania wachimbaji wake wadogo kule katika jimbo lake ya kwamba, ratiba ilishapangwa. Taasisi yetu husika imeanza kuzunguka katika Kanda ya Ziwa tunavyoongea wanatoa mafunzo mbalimbali. Na mwaka huu wa fedha kabla haujaisha watakuja pia na Mbeya na GST nao wale wanaofanya mambo ya jiolojia watakuja kutoa semina katika mwaka ujao wa fedha ya jinsi ya kuchukua sampuli na jinsi ya kutambua maeneo yenye madini kwa ajili ya kunufaisha wachimbaji wadogo. Ahsante sana. (Makofi)