Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 12 Energy and Minerals Wizara ya Madini 140 2022-02-16

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza kuwasaidia Wachimbaji wadogo wa madini katika Mji wa Njombe kama inavyofanya kwenye maeneo mengine?

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Deodatus Philip Mwanyika, Mbunge wa Jimbo la Njombe Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuwasaidia wachimbaji wadogo Wizara kupitia Shirika la Madini la Taifa imeandaa mkakati maalumu kwa ajili ya kuwasaidia na kuwaendeleza wachimbaji wadogo nchini ikihusisha wachimbaji waliopo Mkoani Njombe, pia. Mkakati huo ambao umeanza kutekelezwa mwaka wa fedha 2021/2022 umejikita kwenye maeneo manne muhimu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, eneo la kwanza ni Mpango wa Mafunzo (Training Calendar) kwa mwaka mzima ambao utafanyika nchi nzima. Mpango huo uliandaliwa kwa kushirikisha wachimbaji wadogo kupitia uwakilishi wa vyama vyao (FEMATA) na ambao kwa sasa upo tayari kwa utekelezaji. Mafunzo haya yatatotelewa kwa kuhusisha Taasisi mbalimbali zinazohusika na utozaji wa kodi na tozo mbalimbali kama vile Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Tume ya Madini pamoja na Halmashauri zetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mpango wa pili ni Mpango wa kuwawezesha wachimbaji wadogo kukopesheka katika taasisi za fedha ambapo tayari Shirika limeishaingia makubaliano na Taasisi za fedha za ikijumuisha CRDB, NMB na KCB ambazo zipo tayari kuwakopesha wachimbaji hao.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mpango wa Tatu ni Kuingia makubaliano na GST (Geological Survey of Tanzania) taasisi yetu ya jiolojia, ambayo itawasaidia wachimbaji wadogo kujua taarifa za mashapo katika maeneo yao kabla hawajaanza kuchimba.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mpango wa Nne ni Kupata mitambo ya uchorongaji mahususi kwa ajili ya wachimbaji wadogo na kwa kuanzia Shirika limeagiza mitambo 5 ya uchorongaji mahususi kwa ajili ya wachimbaji wadogo. Ahsante sana. (Makofi)