Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Rehema Juma Migilla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Primary Question

MHE. REHEMA J. MIGILLA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza mchakato wa Wilaya ya Urambo na Kaliua kutumia line yake ya umeme ili kupunguza au kumaliza tatizo la kukatika kwa umeme katika Wilaya hizo?

Supplementary Question 1

MHE. REHEMA J. MIGILLA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, pamoja na majibu haya mazuri ya Serikali tunaomba yasiishie kwenye maandishi, tunataka kwa vitendo na kwa muda husika, lakini nina maswali madogo mawili ya nyongeza, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ilitutangazia bei, hasa sisi watu wa vijijini kwamba, gharama ya kuunganisha umeme ni 27,000/= lakini haikuweka wazi hiyo 27,000/= inajumlisha nini na nini. Sasa tunataka tufahamu;

Je, Serikali inaposema 27,000/= inajumuisha na nguzo bila kuangalia umbali wa mlaji wa mwisho? Kwa sababu, maeneo mengi unalipa 27,000/= lakini hawapelekewi umeme na kila wakiuliza wanaambiwa tatizo ni nguzo, tunataka leo utupe maelezo yanayojitosheleza kuhusu hili tatizo?

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini swali langu la pili. Kumetokea mabadiliko ya ghafla sana na ya kimyakimya kuhusu bei ya umeme kulingana na units ambazo mnazitoa. Hapo nyuma wananchi walikuwa wakilipa 10,000 wanapata units 78, lakini sasa hivi mabadiliko haya yameasababisha 10,000 hiyo hiyo wanapata unit 28. Sasa je, tunataka tufahamu nini kimesababisha haya mabadiliko ya kimyakimya kwa hizi units ambayo inawatesa sana hawa wananchi wetu ambao ni masikini? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Rehema, Mbunge wa Ulyankulu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika eneo la kwanza niombe kutoa maelezo mazuri kabisa fasaha kwa niaba ya Serikali kwamba, ukilipa 27,000/= utaletewa umeme ulipo pale kijijini, hata kama ni kwa nguzo 20, ni nguzo moja, ni bila nguzo, maelekezo ya Serikali, gharama ya kuunganisha umeme kwa kijijini ni 27,000/=. Na mara nyingi unapounganisha umeme utahitaji mita, utahitaji nguzo, utahitaji waya, utahitaji transformer pia, ni 27,000/=.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama kuna maeneo ambapo tunapata matatizo Waheshimiwa Wabunge, basi tuwasiliane ilki msimamo huu wa Serikali uweze kutekelezwa katika maeneo ambayo yanahusika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini katika eneo la pili, kwa taarifa zilizopo, mabadiliko ya bei za umeme ya mwisho yalifanyika mwaka 2016 kwa kanuni zilizotolewa na msimamizi wa bei ambae ni EWURA. Mpaka sasa hatuna taarifa na hatuna maelekezo na hatuna mabadiliko yoyote yale kwenye gharama za umeme. Lakini wale watumiaji wadogo, tunawaita Domestic 1, maarufu D 1, ukiwa na 9,150/= utapata unit 75, lakini kama utatumia zaidi ya unit 75 kwa mwezi unakidhi kutoka kwenye D 1 kwenda T 1 hivyo, 9,150/= haiwezi kununua tena unit 75 unakuwa ume-graduate kwenda kwenye matumizi makubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, niombe kama kuna Waheshimiwa Wabunge ambao wananchi wao bado wanatumia unit 75 na pungufu kwa mwezi, lakini gharama za ununuzi wa umeme zimebadilika kwao, basi tuwasiliane ili tuweze kubaini tatizo ni nini, tuondoe hilo tatizo, lakini hakuna mabadiliko ya wazi wala ya kimya ya gharama za umeme. Nashukuru.

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. REHEMA J. MIGILLA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza mchakato wa Wilaya ya Urambo na Kaliua kutumia line yake ya umeme ili kupunguza au kumaliza tatizo la kukatika kwa umeme katika Wilaya hizo?

Supplementary Question 2

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa nafasi, nami niulize swali dogo la nyongeza: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Nkansi ni miongoni mwa wilaya ambazo zinapata umeme kwa muda mfupi sana. Wizara ya Nishati ilisema wanaweza kuondoa tatizo hilo kwa kutuunganisha kwenye gridi ya Taifa kwa hiyo, tunatumia umeme kutoka Zambia.

Nataka kujua kama Wizara bado inaamini mpaka leo kwamba, kuunganishwa kwenye gridi ya Taifa ndio suluhisho, ni lini mtatuunganisha kwenye gridi ya Taifa?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Aida Khenani, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatekeleza miradi miwili kwa pamoja ya kupeleka gridi ya Taifa katika Mkoa wa Katavi na Kigoma kwa pamoja. Na gridi hiyo ya Taifa inatarajiwa kufika maeneo hayo ifikapo Oktoba mwaka huu. Na itakapokuwa imefika Katavi ndio sasa tutakamilisha mpaka maeneo mengine ya Jirani ambayo hayana gridi ya Taifa.

Name

Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. REHEMA J. MIGILLA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza mchakato wa Wilaya ya Urambo na Kaliua kutumia line yake ya umeme ili kupunguza au kumaliza tatizo la kukatika kwa umeme katika Wilaya hizo?

Supplementary Question 3

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa nini Serikali isiiondoe Wilaya ya Meatu kuchukulia umeme katika Kituo cha Mabuki, Mwanza, chenye umbali wa kilometa 200 ikairejesha Wilaya ya Meatu ilikokuwa mwanzo inachukulia Ibadakuli, Shinyanga, umbali wa kilometa 100 ili kuondoa tatizo la kukatikakatika kwa umeme, ambalo linasababishwa na umeme kusafiri umbali mrefu?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Leah Komanya, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kuweka eneo moja kupata umeme kutoka sehemu nyingine ni jambo la kitaalamu na sio kwa kuangalia umbali peke yake, lakini pia na uwezo wa kituo fulani kuhudumia watu wetu walioko jirani, lakini naomba nikiri kwamba, nachukua jambo hilo na nitaenda kuliwasilisha kwa wataalam ili walichakate na kuona kama kwa sasa tunaweza kuhama kutoka upande hu una kwenda kwingine, kwa ajili ya kuboresha huduma hii. (Makofi)

Name

Hassan Seleman Mtenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. REHEMA J. MIGILLA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza mchakato wa Wilaya ya Urambo na Kaliua kutumia line yake ya umeme ili kupunguza au kumaliza tatizo la kukatika kwa umeme katika Wilaya hizo?

Supplementary Question 4

MHE. HASSAN S. MTENGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru.

Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo la Mtwara Mjini ni jimbo ambalo kwa sasa linaongoza kwa ukatikaji wa umeme kwa kila siku, mikatiko inaweza ikafika zaidi ya 30 kwa siku. Je, ni lini Serikali itaiingiza Mtwara na Lindi kwenye gridi ya Taifa na sisi tukafaidika na umeme wa gesi ambayo inatoka Mtwara?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Mheshimiwa kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mtenga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza niwashukuru wana- Mtwara kwa kuwa, sehemu kubwa sana ya umeme ambayo inalisha nchi hii kwenye gridi ya Taifa inatokea katika Mkoa wa Mtwara. Na nimuahidi kwamba, katika mipango ambayo Serikali ikonayo ni kuhakikisha kwamba, sasa umeme ambao unazalishwa tayari kwenye gridi ya Taifa na kwenyewe uweze kufika. Niseme kwenye mipango tuliyokuwanayo kufikia 2025 itakuwa imefikia hatua sasa ya kuamua ni lini gridi ya Taifa itafika katika Mkoa wa Mtwara na Mkoa wa Lindi kwa ajili ya kufikisha huduma nzuri zaidi.

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. REHEMA J. MIGILLA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza mchakato wa Wilaya ya Urambo na Kaliua kutumia line yake ya umeme ili kupunguza au kumaliza tatizo la kukatika kwa umeme katika Wilaya hizo?

Supplementary Question 5

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa, Wilaya ya Ki- TANESCO ya Ukerewe inapata umeme kutoka kwenye kituo cha kupoza umeme kilichoko Bunda, ambako ni umbali mrefu, hali inayosababisha kutokuwa na umeme wa uhakika. Na kwa kuwa Serikali ina mpango wa kujenga vituo kadhaa vya kupoza umeme kwenye maeneo mbalimbali nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kwa nini sasa Serikali isiweke Ukerewe kama moja ya maeneo ambayo yatajengewa kituo cha kupoza umeme, ili kurahisisha umeme wa uhakika kwenye eneo la Ukerewe? Nashukuru sana. (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mkundi, Mbunge wa Ukerewe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, niombe kulichukua jambo hili, ili wataalam waende wakachakate na kuona economic feasibility ya kuweka kituo pale Ukerewe na uwezo wa kukitumia katika mahitaji tuliyonayo, ili kuweza kuboresha huduma ya umeme katika eneo la Ukerewe.